Trending News>>

CR7 pamoja na kocha wake, ligi yake, timu yake na wakala wake waziteka tuzo za Global

Huu ni mwaka wa neema kwa Mreno Cristiano Ronaldo kwani pamoja na kwamba Real Madrid hawafanyi vizuri lakini haikumzuia kubeba tuzo ya mwanasoka bora wa dunia tuzo za Dubai Global Soccer.
Wakati CR7 akibeba tuzo hiyo, ligi anayoshiriki Cristiano Ronaldo ya La Liga imezibwaga ligi za EPL, Serie A na Bundesliga kwa kuibuka kama ligi bora zaidi kwa mwaka 2017 huku timu ya CR7 Real Madrid wakiibuka kuwa timu bora 2017.
Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane ambaye pia ni kocha wa Ronaldo alitwaa tuzo ya kocha bora huku wakala wa Ronaldo Jeorge Mendez akiibuka kidedea kama wakala bora wa kwa mara ya saba wachezaji kwa mwaka 2017.
Gwiji wa zamani wa Italia Fransesco Totti alitwaa tuzo ya heshima kwa wachezaji huku kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Italia Marcelo Lippi akitwaa tuzo ya heshima kwa upande wa makocha.
Tuzo ya kocha bora imeenda kwa kocha wa nchini Ujerumani Felix Brych huku Hector Cuper baada ya kuisaidia Misri kwenda katika fainali za kombe la dunia amepewa tuzo ya kocha bora wa nchi za kiarabu.

No comments:

Powered by Blogger.