Trending News>>

Mwakyembe apigilia msumari TFF


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amefunguka na kupigilia msumari jambo ambalo linaendelea (TFF) na kusema ni muendelezo ya kampeni ya serikali ya awamu ya tano kusafisha kila sehemu na kuleta uadilifu.
Mwakyembe amesema serikali ya awamu ya tano imeamua kusafisha kila kona na kufikia sehemu zingine ambazo zilikuwa haziguswi ndiyo maana kuna baadhi ya viongozi wa michezo nchini wamefikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.
"Kama ni mabadiliko mimi nimeridhika nayo tunakwenda mbele nimefurahi kwamba kulikuwa na vikwazo viwili vitatu saizi vimeondoka tutafanya uchaguzi kama ilivyopangwa na nina uhakika tutapata timu nzuri ya kuongoza mchezo wa soka nchini. Mimi naomba Watanzania watuelewe kitu kimoja nchi nzima iko katika kampeni ya kuondoa ubadhilifu, wizi, udokozi, rushwa katika maeneo yote, haiwezekani tukawa na kakisiwa hapa Tanzania hakafikiwi, hakashikiki wala hakaguswi ambapo kila mtu anajua nikiwa pale siguswi haiwezekani hilo kwa serikali ya awamu ya tano" alisisitiza Mwakyembe 
Mbali na hapo Mwakyembe aliendelea kusema kuwa kushirikiliwa kwa baadhi ya viongozi wa TFF na vyombo vya dola si kwamba serikali inampango wa viongozi hao kutogombea katika nafasi mbalimbali bali serikali inafuata sheria hivyo hawawezi kusema jinai isubiri mpaka uchanguzi ufanyike.
"Kinachoendelea sasa hivi ni kampeni ya serikali kuhakikisha kuwa kunakuwa na uadilifu mkubwa katika kila kitu ambacho tunakifanya, sasa hawa viongozi wa Simba wana uchaguzi gani kesho? Hata kesho mtu mwingine yoyote ataingia humo mimi sijawahi kuona hata simu moja sheria inayosema kama kuna uchaguzi basi sheria ya jinai isimame mpaka uchaguzi ufanyike, hiyo mimi sijawahi kuona. Kichanofanyika ni kampeni ya kawaida kabisa kuhakikisha katika nchi yetu hakuna tena sehemu ambazo ndiyo uchafu unatupwa huko" alisisitiza Mwakyembe 
Mbali na hilo Mwakyembe ameonyesha wasiwasi kuwa fedha ambazo Watanzania walichanga kwa ajili ya timu yao ya Serengeti Boys ilifanyiwa hujuma na kupigwa na baadhi ya viongozi wa soka na kusema kwa sasa wapo kwenye mpango wa kufanya uchunguzi kubaini hilo na kujua ni wapi walikosea mpaka pesa hizo zimeweza kupigwa na wajanja.

No comments:

Powered by Blogger.