Trending News>>

Kipa wa Serenegti Boys amefanya kosa kama la Manyika Jr

HIVI karibuni, kipa mkongwe wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Manyika Peter alieleza namna alivyoamua kuchukua uamuzi mgumu kwa mwanaye kipa, Peter Manyika.
Mzazi huyo ambaye ni mmoja wa wachezaji wachache wa Tanzania waliowahi kucheza nje ya Tanzania, alieleza jinsi ambavyo hafurahishwi na mwanaye kutopata nafasi katika klabu yake ya Simba.
Manyika aliwahi kucheza Shelisheli, Iran pia lakini amewahi kuwa kocha wa makipa katika timu ya Ligi Kuu nchini Oman ya Seeb.
Wakati akielezea uamuzi wa kumshawishi mwanaye aachane na Simba, Manyika alielezea namna ambavyo amekuwa hapati nafasi ya kucheza na kusisitiza umefika wakati wa kuangalia nafasi ya kucheza kuliko fedha au mshahara mkubwa.
Anaamini kwa umri alionao mwanaye ni jambo gumu kuendelea kukaa benchi huku akipata fedha. Anaona hivyo si kuujali mpira na mapenzi yake au kutoangalia maendeleo na mwisho anaona bora acheze timu ndogo inayompa nafasi ya kucheza kuliko kupokea mshahara mkubwa huku akiwa benchi Simba.

No comments:

Powered by Blogger.