Trending News>>

Maisha magumu ya chumba kimoja ya Cristiano Ronaldo na dada zake enzi hizo

June 14 2017 naomba nikuletee historia ya mchezaji bora wa Dunia kwa mara nne Cristiano Ronaldo ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Ureno na anaichezea Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo, inawezekana hujui historia ya Cristiano Ronaldo mtu wangu naomba nikuletee historia yake ya utoto.

Jina lake kamili ni Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro alizaliwa February 5, 1985 Funchal, Madeira kisiwa kidogo kilichopo pwani ya Magharibi Ureno, Ronaldo ni mtoto wa nne katika watoto wanne waliyozaliwa katika familia ya Maria Dolores dos Santos na Jose Dinis Aveiro.

Jina la Ronaldo lilitokana na baba yake kumpenda sana aliyekuwa Rais wa 40 wa Marekani Ronald Reagan, maisha ya utoto ya Cristiano Ronaldo yalikuwa na changamoto nyingi na maisha magumu, baba yake Jose Dinis Aveiro kazi yake ilikuwa ni kutunza bustani na alifariki mwaka 2005 kwa matatizo ya figo yalitokana na ulevi wa kupindukia.

Ronaldo akiwa na baba na mama yake
Mama yake mzazi Maria Dolores dos Santos ili kuweza kuimudu na kuitunza familia yake alikuwa akifanya kazi kama mpishi na mfanyaji usafi, kitu ambacho maisha yalikuwa magumu enzi hizo na kupelekea Ronaldo, kaka yake na dada zake wakubwa wawili walilazimika kushea chumba kimoja katika umri ambao hawakupaswa kwa dada na kaka kushea chumba.

Ronaldo akiwa na kaka yake Hugo Aveiro na dada zake Katia Aveiro na Elma Aveiro
Ronaldo alianza kucheza soka katika timu ambayo baba yake Jose alikuwa akifanya kazi kama mtunza vifaa wa timu hiyo, wakati huo Ronaldo alikuwa na umri wa miaka 10, baadae akaingia katika timu za Nacional ya Madeira na akafanikiwa kuingia katika Academy ya Sporting CP timu iliyomtoa.

Mwaka 2002/3 akafanikiwa kuichezea Sporting CP timu B na baadae akaingia timu ya wakubwa, kingine ambacho hufahamu Cristiano Ronaldo akiwa na umri wa miaka 15 aliwahi kufanyiwa upasuaji baada ya kugundulika kuwa na tatizo la racing heart.

Cristiano Ronaldo alikuwa maarufu shuleni kwa wanafunzi wenzake na alifukuzwa shule baada ya kumtupia kiti mwalimu, Ronaldo hadi leo huwa anakiri kufanya kosa hilo lakini anaamini mwalimu alimkosea heshima ndio maana alifanya hivyo kwa hasira.

Baada ya kufukuzwa mama yake Maria akamwambia hakuna namna ni kuongeza bidii katika soka pekee ndio kunaweza kumkomboa katika maisha, ugumu wa maisha uliwahi kumfanya mama Ronaldo ahisi kuwa mwanae anaweza kuingia katika matumizi ya madawa.


Alipojiunga na Andorlinha

“Nilipokuwa mdogo niliwahi kumwambia baba yangu kuwa sisi tutakuwa matajiri na tutakuwa na nyumba kubwa, aliniambia hiyo haiwezekani, leo hii ninachokile nilichoahidi kwa baba yangu lakini ndio sipo nae tena” >>>> Cristiano Ronaldo

No comments:

Powered by Blogger.