Trending News>>

MICHEZO:Lukaku kucheza dhidi ya Abdi Banda na Kelvin Yondani.


Sasa ni wakati wa timu kujiandaa kwa ajili ya msimu wa ligi wa mwaka 2016/2017, hii ni baada ya ligi kuu takribani zote kuwa zimeshamaliza ligi katika mataifa yao.
Jambola kutia moyo na kusisimu ni kwamba klabu ya Everton imetoa taarifa rasmi kwamba katikati ya mwezi ujao watakuwa klabu ya kwanza EPL kuja Africa Mashariki.
Wakiongozwa na mshambuliaji wao hatari Romelu Lukaku Everton watafika katika ukanda wetu wa Afrika na kati ya nchi zitakazotembelewa ni nchi yetu ya Tanzania.
Hii ina maana vilabu vyetu vitapata nafasi ya kujipima nguvu dhidi ya klabu hiyo,Yanga na Simba wanaweza kupata nafasi kucheza na timu hiyo kongwe toka nchini Uingereza.
Tayari kupitia ukurasa wao wa Twitter, klabu hiyo imetoa taarifa rasmi kwamba katika maandalizi ya msimu ujao wa ligi watakuja katika ukanda wa Afrika Mashariki kujiweka sawa.
Katika msimu uliomalizika wa ligi, klabu ya Everton ilifanikiwa kumaliza katika nafasi ya saba ikiwa ni nafasi moja chini ya mabingwa wa Europa klabu ya Manchester United.

No comments:

Powered by Blogger.