Trending News>>

Habari kwa mashabiki wa Manchester United.


Baada ya lawama na maneno mengi kuhusu kiungo Paul Pogba sasa kocha wake Jose Mourinho ameibuka na kumtaftia dawa ambayo ana uhakika akiipata itawafanya mashabiki wamshangilie Pogba kila wakati.
Mourinho baada ya kuumizwa kichwa kwa muda mrefu sasa anaona kiungo wa PSG Blaise Matuidi ndio muarobaini wa tatizo na kiwango cha Pogba, Mourinho anataka kumleta Matuidi Old Trafford ili kujaribu kumchezesha pembeni ya Paul Pogba.
Lakini achilia hayo ya Pogba, kuna habari ambazo sio nzuri sana kwa mashabiki wa klabu ya Manchester United kwani klabu ya Barcelona imepiga hodi katika timu hiyo ili kuchukua mchezaji wao muhimu.
Taarifa zinasema klabu ya Barcelona imetuma maombi rasmi katika klabu hiyo ili kuona uwezekano wa kumsajili kiungo wa timu hiyo Ander Herrera ambaye amekuwa na msimu mzuri sana na Manchester United.
Wakati huo huo Pierre Aubemayang ambaye United wanamtaka kwa dau la £40m inasemekana amewaambia mabosi wake wa Borussia Dortmund kwamba anataka kuondoka katika klabu hiyo.
Lakino pia Manchester United hao hao wameanza mchakato wa kumnunua Andrea Belotti kutoka Torino ambapo wanaamini wakimnunua Belotti na Griezman watakuwa na safu bora kabisa ya ushambuliaji.

No comments:

Powered by Blogger.