Trending News>>

MAN U UWANJANI LEO, SANCHEZ KAZINI


Alexis Sanchez.
MANCHESTER Unit­ed inatarajiwa kuwa uwanjani leo Ijumaa kuivaa Yeo­vil Town katika raundi ya nne ya Kombe la FA.
United itakuwa ugenini kuivaa timu hiyo ya dara­ja la pili ambapo kuna mambo kadhaa yatakuwa gumzo juu ya mchezo huo.
Alexis Sanchez kuanza kazi
Kocha Jose Mourinho wa United anatarajiwa kuan­za kumtumia staa wake mpya kikosini hapo kwa mara ya kwanza. Hiyo ni kiu ya mashabiki wengi ku­muona mchezaji huyo ka­tika kikosi hicho.
Mourinho mechi 100
Leo ni siku ya ku­zaliwa ya Mourinho ambaye anatimiza umri wa miaka 55 pia atakuwa akifikisha mchezo wake wa 100 akiwa na Man Unit­ed. Ameshinda 61, sare 23 na kupoteza 15, mabao ya ku­funga ni 176, mabao ya kufungwa 70 na ana mataji matatu.
Mabadiliko kikosini
Mourinho anaweza kufanya mabadiliko ya kikosi ikiwemo kumpa nafasi kipa Sergio Romero na kumpumz­i ­s h a David De Gea.
A n d e r H e r r e r a mechi 150
Kiungo h u y u ame s h ­a c h e z a m e c h i 149 aki­wa United k a m a atache­za basi atafiki­sha mechi 150.

No comments:

Powered by Blogger.