Trending News>>

Mzunguko Wa Kwanza England… Mambo Yamekwisha


WIKIENDI ijayo timu zote kwenye Ligi Kuu England zinamaliza mzun­guko wake wa kwanza wa ligi hiyo yenye mshikemshike wa kutosha.
Kila timu imeonyesha kiwango chake, baadhi ya wachezaji wam­eonyesha ubora wao uwanjani huku wengine wakiwa ni wale ambao walikuwa hawatarajiwi kuwika na wengine wakiwa ni wale ambao walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri.
Tayari Man­chester City wameongoz a kwenye mzun­guko huu waki­wa hawajapote­za mchezo hata mmoja kati ya 18 ambayo wa­mecheza hadi sasa.

Wachambuzi wa masuala ya soka wame­shawapa nafasi kubwa ya kut­waa ubingwa, makocha kad­haa wa Ligi Kuu England wame­shawatangaza kama wapinza­ni sahihi wa ubingwa wa England msimu huu.
Kocha Pep Guardiola, am­etengeneza kikosi imara sana ambacho kimeonekana kuwe­za kuteka kila timu kwenye ligi hiyo kwa sasa.
Tayari amefanikiwa kuibuka na ushindi dhidi ya timu zote kubwa kwenye Ligi Kuu England msimu huu, amewafunga Man United, Chelsea, Arsenal, Totten­ham Hortspur pamoja na Liver­pool ambazo zilikuwa zinapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa msimu huu.
Tayari kwenye michezo yao msimu huu imetoka sare mich­ezo miwili tu ikiwa imeshinda 16 na huo mchezo mmoja haijatoka dhidi ya timu kubwa bali ilitoka sare dhidi ya Everton ambapo ili­kuwa sare ya bao 1-1.

Hii inaonyesha kuwa City im­ejidhatiti kwa kiwango cha hali ya juu kwani mpaka sasa imedondo­sha pointi mbili tu.
Wakati wa o wakifanya hivyo timu inayoshika nafasi ya pili, Manchester United yenyewe imepoteza michezo mitatu ambayo ni sawa na pointi tisa na kutoka sare mara mbili ambazo ni sawa na pointi nne, jumla wenyewe wamepoteza pointi 10 kwenye michezo 18 ya mwanzoni mwa ligi
Hata hivyo, City wanawe­za kupoteza, lakini siyo rahisi kwao kudon­dosha pointi kumi na mbili kwenye mzunguko wa pili wa ligi hali ambayo inaonyesha kuwa wanaweza kutangaza ubingwa wa England mapema zaidi mwakani.
Faida nyingine am­bayo City wanayo ni kwamba wachezaj i wao wote m a h i r i wameen­d e l e a kuwa imara, hawajapata mt i k i s i k o m k u b w a kuanzia msimu umeanza.

Mastaa wa timu hiyo Kevin De Bruyne, Raheem Ster­ling na wengine wengi wamebaki kwenye ubora wao, haku­na hata m m o j a amb a y e ameweza k u p a t a majeraha a u kadi am­b a y o imeweza kuwafanya wakakosa mchezo muhimu wa timu hiyo.
City wamekuwa na kikosi kilekile kwa kipindi chote cha msimu mzima, hii ni kama ilivyokuwa kwa Chelsea wakati wanach­ukua ubingwa msimu ulio­pita au nyuma yake wakati Leicester nao hawakuwa na majeruhi wala kadi nyekun­du.

MANCHESTER INAWEZA KU­MALIZA WA PILI
Timu nyingi am­bazo zimekuwa ziki­wania nafasi ya ub­ingwa wa Ligi Kuu England zimekuwa zikifanya vibaya sana kwenye mbio hizo.
United imekuwa ikiwategemea wache­zaji wengi ambao mashabiki wao wa­likuwa hawawategemei kuwa wanaweza kufanya makubwa msimu huu.

Pamoja na Romelu Lu­kaku kufikisha mabao kumi kwenye L i g i K u u E n g l a n d lakini wame­kuwa waki­pata msaada mkubwa kutoka kwa Jesse Lin­gard ambaye ameamka na kufunga mabao manne kwenye michezo mi­tano na kuonyesha kuwa ni msaada mkubwa kwa kocha Jose Mour­inho.
Huku pia timu hiyo ikipata hudu­ma safi kutoka kwa kipa wao David de Gea ambaye amekuwa akiokoa michomo kadhaa ambayo inge­washinda makipa wengine.

Kukosa ubingwa kwa Jose Mourinho hakuwezi kuwa na faida hata kidogo hata kama atamaliza katika nafasi ya pili kwenye ligi hiyo kwa kuwa sasa itakuwa ni miaka mitano bila ubingwa wa England jambo ambalo mabosi hao hawawezi kuvumilia.

Hili linaonekana kuwa pigo kwa Manchester kwa kuwa hawajazoea maisha ya namna hii, hivyo kocha Jose Mourinho kuwafuta machozi basi angalau ana­takiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya jambo ambalo pia linaonekana kuwa gumu kwake.

United ni lazima wa­pambane kama wana­taka kumaliza kwenye nafasi ya pili kwa kuwa inawaniwa pia na Arsenal ambao wapo nyuma yao kwa pointi tisa, lakini kwa mwendo wa timu zote ni rahisi kuwafikia.

Lakini pia inawindwa na Liverpool pamoja na Chel­sea ambazo zote zime­kuwa kwenye mwendo wa kufanana hakuna hata moja ambayo ina uhakika.
Man United wamepote­za michezo mitatu kwenye mechi 18, Liverpool wamepoteza michezo mi­wili, Chelsea wamepoteza minne huku Arsenal wak­ipoteza michezo mitano.
Liverpool wenyewe wamekuwa wakipata msaada tosha toka kwa Mohamed Salah ambaye amekuwa akiwafung­ia kwenye kila mchezo muhimu.

Salah kwa sasa ndiye ki­nara kwenye ufungaji kati­ka Ligi Kuu England akiwa amefunga mabao 14 na anatajwa kuwa usajili bora zaidi msimu huu.

Kwa ujumla mchezaji huyo amefanikiwa ku­funga mabao 20 kwenye michuano yote akiwa ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kusa­jiliwa kwenye msimu wa kwanza na kufunga ma­bao 20 ndani ya kikosi cha Liverpool.
Ameweza kuwazidi mastaa wenye heshima kwenye timu hiyo kama Luis Suarez, Fernando Torres, Michael Owen na Robbie Fowler ambao hawakufika mabao 20 kwa msimu wao wa kwanza.

Kwa upande wa Chel­sea wenyewe kwa sasa wapo nafasi ya tatu na kocha wa timu hiyo Anto­nio Conte, ameshasema kuwa hana presha tena kwa kuwa wameshamaliza mbio za ubingwa.

Kocha huyo amekuwa wa pili kukiri kuwa Man­chester City ndiyo wana­takiwa kutwaa ubingwa huo msimu huu.
Timu hiyo kwa sasa ipo nyuma ya City kwa pointi 14, ambazo zinaonekana ni nyingi sana kuzipindua kwenye mzunguko wa pili wa ligi hiyo.
Kocha huyo amesema siyo kwamba wamefanya vibaya, bali Manchester City wameonyesha uw­ezo wa juu zaidi kuliko ilivyokuwa ikitegemewa mwanzoni mwa msimu huu.

No comments:

Powered by Blogger.