Trending News>>

Mwanamke Kama Unatabia Hii Basi Neno Ndoa Utalisikia Kwenye Bomba

Hivi unajua kwanini mahusiano mengi katika karne hii yanakufa sana ukilinganisha na miaka ya zamani? Nini ambacho kimetokea miaka ya hivi karibuni? Naomba utafakari kwa muda usiopungua dakika tano kisha majibu ubaki nayo.

Binafsi leo sikuja kwa leo ya kuzungumzia sababu hizo, ila leo nataka niseme  na wanawake wote wenye tabia ya kupenda ganda la ndizi kuteleza, unawajua wanawake wenye tabia za aina hii kwa watalam wa masuala ya mahusiano wamewapa jina jipya ambalo ni magolipa.

Wao kazi yao kubwa ni kusubiri wanaume zao waende kutafuta ili hali wao wamekaa nyumbani wakisubiri kuletewa, wanawake wa aina hii kiufupi ukiwachunguza kwa umakini huwa hawana uchu wa mafanikio na maendeleo hata chembe. Na wanawake wa aina hii huwa wana uhusiano mzuri na romote control za tv.

Nataka nikuibie siri wewe mwanadada mwenye tabia ya aina hii, hivi unajua wanaume wengi katika utawala huu wa sizonje  hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani ‘golikipa’? kama ulikuwa hujui basi leo nakupa makavu live.

Hivi unajua  Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa, kusugua miguu akimsubiria mwanaume arudi akutelee, sasa hivi imepitwa na wakati? Kama ulikuwa hujui basi leo nakupa ukweli wako bure pasipo kuchangia hata mia mbovu.

Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

Kabla sijamaliza kicheni part ya  leo nataka kukwambia ya kwamba maisha ni kutafuta, punguza kufanya vitu visivyokuwa wa maana katika maisha yako,punguza muda wa kukaa vibalazan huku macho yakikutoka huku kazi ikiwa ni kuwasema watu wengine.

Wewe ni mtu mzima mwenye meno 32, una akili timamu buana, tafuta shughuli za kufanya ambayo itakufanya uweze kujikiingizia kipato, binafsi naamini unaweza kwani ule msemo wa wahenga wapya ya kwamba wanawake wanaweza upo kwa ajili yako.

Jifunze kupambana na hali yako kama young killer muhasisi ya hip-hop asemavyo. Kukaa ukimsubiri shemela akuletee sio mpango mzima pia nidhambi na chukuzi kwa mwenyezi mungu.

No comments:

Powered by Blogger.