Trending News>>

Msanii mkongwe kwenye Game ya sanaa ya Uigizaji Shamza Ford amempa tahadhari msanii mwenzake Wema Sepetu.


Staa wa Bongo, Wema Sepetu.
KUFUATIA kuhama chama kutoka Chadema kwenda CCM kwa mwanadada kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Wema Sepetu, msanii mwenzake, Shamsa Ford ameibuka na kumtahadharisha pamoja na wasanii wote kwa jumla.

Akipiga stori na Za Motomoto News, Shamsa alisema wao siyo wanasiasa hivyo suala la Wema la kwenda na kurudi kwenye vyama vya siasa inawezekana anapata faida lakini cha muhimu asisahau kazi yake.

“Siwezi kuzungumzia sana suala la Wema kuhama vyama maana ni lake binafsi na huenda lina faida kwake, nawasihi tu wenzangu wasisahau kazi yao ya sanaa iliyowatambulisha kwa jamii,” alisema Shamsa.

No comments:

Powered by Blogger.