Trending News>>

Pretty Afunguka Madai Ya Kutelekeza Ndoa!


Msanii wa filamu Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’.
MSANII wa filamu Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ amefungukia madai ya kuwa, kabla ya kwenda India ‘kudanga’ aliolewa na kuitelekeza ndoa kwa kusema si kweli kama aliolewa.

Akifafanua kuhusu madai hayo yaliyoshika kasi kwenye mitandao ya kijamii, Prety alisema ukweli ni kwamba hakuwahi kuolewa, alikuwa na mwanaume huyo polisi kipindi yupo Mwanza ambaye alikuwa anaishi naye kinyumba lakini waliachana hata kabla ya safari yake ya India.

“Haya ni maneno ya watu wanaotaka kunichafulia CV yangu, huyo mwanaume sikuwahi kufunga naye ndoa ya serikali wala ya kimila, ila niliwahi kuishi naye kinyumba na tulimwagana kabla sijafikiria kwenda India, iweje hayo madai yaibuke leo,” alisema Prety.

No comments:

Powered by Blogger.