Trending News>>

MAJANGA :: Baada ya Samatta Huyu Mwingine wa Kimataifa Kaumia.


Kiungo mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Farid Musa anayecheza soka la kulipwa kwenye klabu ya Tenerufe nchini Hispania amepata majeraha ya goti (knee ligament).
Farid mwenyewe amethibitisha kuwa majeruhi huku kesho akitarajiwa kwenda jijini Madrid kukutana na madaktari bingwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
“Ni kweli nimepata majeraha ya goti, kesho nakwenda Madrid kukutana na doctor kwa ajili ya uchunguzi zaidi”-Farid.
Endapo itathibitika ni majeraha makubwa ya goti, basi huenda akakaa nje ya uwanja hadi mwishoni mwa msimu huu.
Taarifa hii imekuja siku moja baada ya nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta kupata majeraha yatakayomuweka nje kwa kipindi cha miezi sita (6).

No comments:

Powered by Blogger.