​ukiachana na mabeki ambao kwa sasa wengi wao ni wastahafu,  ambao waliweza kumkaba na kumzuia Mchezaji mahiri wa klabu ya Barcelona Lionel Messi asiwe na mazara yoyote,  basi kuna mtu anaitwa Xoana Gonzalez. 

Xoana amejitambulisha na kujipambanua katika hadhira kuwa Messi kwake yeye ni sawa na Kuku kwa Kicheche.  Xoana ni mwanadada mrembo,  ambae ameweka wazi kuwa amewahi kupiga game na msakata kabumbu huyo nyota wa Argentina. 

Mwanadada huyo anasema,  kiukweli ilikuwa ni miaka kadhaa iliopita, na Messi alikuwa ni kijana mdogo,  lakini alifahamu kitu gani Nyota huyo wa Soka amekuwa akifanya,  na hicho kilikuwa kitu muhimu sana. 
Anaendelea kusema siku 1 walinzi wa Messi walimfuata na kumwambia kuwa “kuna mtu anatakiwa kuonana na kufahamiana nae”. 
Akasema kuwa alipigwa na butwaa kwa muda,  ila akajikaza na kwenda mahala alipohitajika kufika.  Anasema hakuamini macho yake baada ya kumuona kiumbe huyo machachari katika medani ya Soka Lionel Andreaz Messi,  akiwa ndie mwenyeji anaetakiwa kuonana nae, “haki nilipigwa na butwaa”. 

“Niliwaza kwa nini amenitumia walinzi wake? Je nina thamani hio? ” na baada ya kufikiri kwa muda aligundua kuwa Messi alikuwa ni mtu mwenulye aibu na mwoga wa mambo ya mapenzi. 
Mrembo huyo akaendelea kuanika kila kilichojiri kati yao, “tulianza kuongelea muziki na akasahau kuwa hajaweka wazi bado kama anae mchumba au hapana.” Lakini baada ya mazungumzo marefu yasio na harufu ya kimahusiano ya mahaba  walisimama na Messi akamuomba mrembo huyo ampeleke kwenye nyumba yake  iliopo Puerto Madero.
binti huyo alishangazwa na kitendo na ombi  hilo la Messi. Anasema alitegemea Messi ndie angemrudisha binti huyo nyumbani kwake lakini akajiuliza kulikoni Messi aanze yeye kurudi nyumbani kabla ya mrembo huyo? 
Mrembo huyo anasema kuwa akavumilia tena utofauti uliojionesha tangu akutane Muargentina huyo. Na walipofika nyumban kwa Messi akashuhudia kituko kingine,  anasema alipofika nyumbani kwa Messi,  basi mchezaji huyo alimkaribisha na kisha akajitambulisha yeye na kazi yake anayofanya. Baada ya hapo,  Messi alivua flana yake na kisha kwenda kumkumbatia na kumuomba msamaha.
Mrembo huyo huku akiwa anacheka,  akasema kuwa Messi alimwambia kuwa alikuwa anampenda tangu zamani,  na alikuwa na hamu siku moja aje alale nae kitanda kimoja,  hivyo anaomba siku hio iwe imewadia.
Xoana anasema kwa upande wake siku hio yote kwake ilikuwa ni ya mshangao mno,  maana alikutana na mtu ambae hakumtarajia na pia mtu huyo aliongea vitu ambavyo hakuvitarajia. 
Mrembo huyo anasema alimuuliza Messi swali moja tu,  “kwanini unataka iwe haraka hivyo? ” ndipo Messi akajibu kwa upole na sauti ya huruma kuwa muda mfupi baadae nitaanza safari ya kurejea Spain. 
Binti huyo anasema kwa jinsi siku ilivyoanza na ushindi kwa mchezaji huyo basi aliamua tu kuifanikisha siku hio iendelee tu kuwa ya ushindi mwanasoka huyo,  hivyo alikubaliana na ombi la Messi na kisha wakaongozana mpaka chumbani.  Mrembo huyo anasema Messi alikuwa ni mwenye papara mno,  kiasi kwamba ilimlazimu mrembo huyo kuangua kicheko muda mwingi.
Na wakati maelezo yake yakitarajiwa kufikia tamati,  binti huyo aliinamisha kichwa chini na kusikitika sana. Na aliponyanyuka akasema kuwa baada ya muda wa dakika kadhaa za kuwa kitandani hapo ndipo shughuli ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu na mwanasoka huyo ikaanza.
Huku akiwa na uso uliojaa dharau na akiongea kwa nyodo iliopitiliza,  mrembo huyo akamaliza kwa kueleza kile alichokishudia na kupambana nacho.
Mrembo huyo akafungua kinywa chake na kusema “When one plays across the whole pitch, you expect someone to return the favour. I wanted him to show me more than that,  one point I felt like I was with a dead body”.