Trending News>>

Meli mbili zafungiwa Jijini Mwanza


Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) mkoani Mwanza imesimamisha usafiri wa meli mbili zinazotoa huduma ya usafiri wa abiria kati ya jiji la Mwanza na baadhi ya visiwa vilivyopo ndani ya ziwa Victoria kutokana na ubovu wa meli.
Mbali na hilo (SUMATRA) imeagiza wamiliki wa meli zingine tatu ikiwemo Mv Clarias inayomilikiwa na serikali kufanya matengenezo ya meli zao kwa haraka iwezekanavyo ili kuendelea kutoa huduma ya usafiri ulio salama kwa abiria na mali zao.  

No comments:

Powered by Blogger.