Trending News>>

Kichanga chateketea kwa moto


Mtoto Faraja Simon mwenye umri wa mwezi mmoja amefariki dunia baada ya chumba alicholazwa kuteketea kwa moto katika Kijiji cha Mbela, wilayani Misungwi mkoani Mwanza.
Akizungumza na wanahabari leo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea juzi Juni 18, 2017 saa 1:00 jioni, ambapo amedai kuwa marehemu alikuwa akiishi kwa mama mlezi aliyefahamika kwa jina Bi. Eva Mnari (37) baada ya kufiwa na mama yake mzazi mwezi uliopita.
Kamanda Msangi amesema siku ya tukio hilo mama mlezi alimlisha mtoto huyo chakula na kisha kumpeleka chumbani kulala na kutoka nje kuendelea na shughuli nyingine.
Amesema wakati mama huyo akiwa nje, aliona moto na moshi mwingi ukitokea chumbani alimolala marehemu ndipo aliita watu waje kumsaidia kuuzima moto huo lakini moto ulikuwa umeunguza godoro alilokuwa amelazwa marehemu na kumuunguza hali iliyopelekea marehemu kupoteza maisha papo hapo
Kamanda Msangi ameendelea kusema kuwa mpaka sasa bado chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na kwamba upelelezi unaendelea kwa kushirikiana na taasisi nyingine za serikali kuhusiana na tukio hilo
Powered by Blogger.