Trending News>>

SIMULIZI :: Jini Mahabati Sehemu ya Tatu (Kwa wenye miaka 18+)

 

SIMULIZI : JINI MAHABATI
SEHEMU YA TATU
MTUNZI:MANYAMASON
AGE: 18+
“Sasa atakuwa ni nani mbona na milango imefungwa” aliwaza Radhia kabla ya kukimbila bafuni na kujimwagia maji na kujisafisha vizuri.
Akajisafisha vizuri na kurudi kulala. Wakati analala akaanza kusika harufu nzuri ya marashi ambayo yalikuwa yakivutia sana kwenye pua zozote za mwanadamu. Si hivyo tu bali ulipuliza upepo mwanana utazani alikuwa ufukweni. Radhia akabaki anashangaa kabla ya kuamua kubadilisha yale mashuka yaliyokuwa yametapakaa damu. “Au itakuwa ni damu ya hedhi” alijiuliza Radhia huku ile harufu ya marashi ikiendelea kunukia.
“Hapana lakini damu ya siku zangu huwa haiwi hivi” alijijibu Radhia na kuhisi kabisa atakuwa amepoteza bikira yake kwenye mazingira ya kutatanisha. Akajipa ujasiri wa kike kisha akabadilisha mashuka na kuweka mengine kisha akapanda kitandani na kulala.
Alilala kwa wasiwasi sana siku hiyo kabla ya kupata usingizi na kumwota yule kijana aliyekutana naye kule chuoni yaani Tariq. Aliota  amezama kwenye penzi zito la kijana huyo lakini wakawa wanapishana sana kauli kwa sababu kijana huyo alisema kuwa Radhia sio yule wa mwanzoni bali ni jinni tena jinni mahabati.
Ndoto hiyo inampleka Radhia mpaka kwenye viumbe vya ajabu na kuonesha kuwa kweli hata yeye si binadamu wa kawaida maana aliweza kuwaelewa viumbe hivyo. Lakini hata Tariq na yeye basi atakuwa ni jini ameyajuaje mambo haya yote na kunileta huku aliwaza Radhia..
Aliaamka huku akihisi kabisa kulikuwa na maumivu makali sana sehemu zake za siri. Ilikuwa ni tayari asubuhi na alikuta kuna barua kwenye meza yake iliyosomeka hivi. “Hongera sana Radhia umekuwa miongoni mwa viumbe wenye uwezo wa kibinadamu na pia uwezo wa kimalaika” kwa kusoma tu ujumbe huu ni kwamba umeridhia kama lilivyo jina lako Radhia maana yake huu radhi na umeridhia au umeridhiwa.
Baada ya kumaliza kusoma tu hicho kikaratasi kikapeperuka na kupotea hapo hapo chumbani. “Mungu wangu mbona si elewe elewi” aliwaza Radhia huku akifungua mlango wake. Akatoka nje kama mtu aliyechachawa kabla ya kurudi ndani na kujiandaa kwa kwenda chuoni.
Alifika chuoni na kuendelea na masomo japo mawazo ya ndoto ile yalikuwa bado yakimchanganya sana akajikuta anaamua kuacha vipindi na kurudi zake hosteli. Alihisi mabadiliko makubwa sana kwenye mwili wake. Alikwenda moja kwa moja kwenye kioo na kujiangalia.
Radhia alizidi kujishangaa kwa sababu kulikuwa na mabadiliko makubwa sana kwenye mwili wake. “Jamani mbona nimezidi kuwa mrembo hata yale madoa madoa ya chunusi siyaoni tena” alijkuta akijuiliza na kujishangaa. Khaa yaani ngozi yangu imelainika na kuwa laini kama ya mtoto mdogo alizidi kupagawa na asiamini kama kweli huyo anayejiona kwenye kioo ni yeye.
Basi hiyo siku ikaisha huku akishinda ndani akiangalia movie huku kioo kikiwa pembeni yake na kila baada ya mda Fulani alikuwa akijiangalia. Hatimaye usiku ukainga akatafuta chakula cha kununua nje kidogo ya hostel hiyo akarudi zake ndani akala na kulala.
Usiku kama kawaida akaanza tena kuota ndoto za mapenzi. Safari hii aliota akifanya mapenzi na yule mwalimu wa usaili yule ambaye lichachawa na kupagawa alipomwona binti huyo. Si unakumbuka mwalimu mpaka akajikuta akiomba namba za Radhia kwa kisingizio kuwa fomu yake ilikuwa imekosewa.
Ndoto ikawa tamu sana na akajikuta anapiga kelele za kimahaba. Radhia alikuwa ulimwengu mwingne sana ambao kelele zake zilifika mpaka kwenye vyumba vya wapangaji wengine. Utamu huo wa ndoto baadaye ulimshtua binti huyo na akaamka na kama kawaida yake alikimbilia bafuni kwenda kuoga. Akajisafisha vizuri huku akijiuliza kwa nini tangia aanze kuishi kwenye nyumba hiyo kuna mambo ambayo hayaelewi.
Akaamua kupotezea na kupanda kitandani na kulala. Alipojifunika shuka tu alisikia kama mtu anagonga mlango. “Eeeh atakuwa ni nani tena usiku huu” aliwaza Radhia na kuinuka na kusogea mlangoni. “Wewe binti vipi kuna usalama?” ilikuwa ni sauti ya baba mwenye nyumba.
“Mimi hata sielewi” alijibu Razia kwa upole. “Ebu fungua kwanza tujue ni nini kinaendelea” aliendelea kusema baba mwenye nyumba. Radhia ama binti kisuara akavuta shuka lake akajitanda vizuri maana alikuwa uchi wa mnyama. Akafungua mlango akakutana na baba mwenye nyumba ambaye na yeye alikuwa amejifunga taulo tu.
Mwanga wa taa wa chumba cha Radhia ulitosha kabisa kufanya baadhi ya mautamu yake kuonekana na mzee baba mwenye nyumba alijikuta akilamba lamba midomo yake kwa uchu wa tamaa mara baada ya kuona jinsi binti huyo alivyokuwa amejaliwa vitu hadimu. Nimesikia kama unapiga kelele za mtu kukubaka na nimesikia kabisa unasema unabakwa aliuliza baba huyo huku akijitahidi kurudisha mtarimbo wake pembenii ambao ulishasimama na kuanza kuleta fujo.
*ITAENDELEA**💋💋💋

No comments:

Powered by Blogger.