Albert Msando Ajiuzulu......Ni Baada ya Video Yake Chafu Kuvuja Mtandaoni
Aliyekuwa
 mshauri wa Chama cha ACT Wazalendo, Albert Msando amejiuzulu nafasi 
yake hiyo kufuatia video chafu zilizomuhushisha kuvuja kwenye mitandao 
ya kijamii hivyo ameamua kujiuzulu ili kuwajibika na kuomba radhi kwa 
wananchi kwa kitendo hicho
Kiongozi
 wa Chama Cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe, amethibitisha kupokea barua 
hiyo na kukubaliana na kiongozi huyo kwa kitendo chake hicho cha 
kuwajibika kisiasa huku akieleza kuwa, Bw. Msando amekuwa na mchango 
mkubwa katika Chama chao. 
"Nimepokea
 barua ya Wakili Albert G. Msando kuomba kujiuzulu nafasi yake ya 
Ushauri wa Chama chetu cha ACT Wazalendo. Ndugu Msando anawajibika Kwani
 anapaswa, nanukuu kutoka katika barua yake, "kuishi Kama mfano Kwa 
jamii inayonizunguka". 
"Ndugu
 Albert Msando amekuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa katika chama 
katika nafasi mbalimbali alizoshika ndani ya chama. Chama kinamshukuru 
kwa moyo wake wa uzalendo na mchango alioutoa katika Chama. Ni matumaini
 yetu ataendelea kushirikiana nasi katika ujenzi wa chama kwa kadri 
atakavyoweza na atakapohitajika kama mwanachama"- alisema Zitto Kabwe.
Zitto Kabwe pia ametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi wamsaidie katika jambo hilo analopitia saizi 
"Nikiwa
 Kiongozi wa Chama nimekubali kuwajibika kwake na kumtakia kheri katika 
kujisahihisha kwake. Ndugu Msando Alberto ameomba msamaha Kwa jamii kwa 
uwazi na ni wajibu wetu kumsaidia kupita katika mitihani iliyomkumba" alimaliza Zitto Kabwe.

No comments:
Post a Comment