Trending News>>

Alichokiandika Idris Sultan kwa Diamond na Watanzania Kwa Ujumla Kuhusu AFCON


Mtanzania Diamond platnumz alipata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye upande wa burudani kwenye ufunguzi wa mashindano ya AFCON ambapo alikabidhiwa bendera ya Tanzania na Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, Nape Nnauye.

Baada ya hapo kulikuwa na maoni tofauti pamoja na maswali kwanini amepewa bendera ile. Idris Sultani ametumia ukurasa wake wa Instagram kumpongeza Diamond kwa kuiwakilisha nchi vizuri huku akiwasii watanzania kusupport wasanii wa nyumbani kwani wanapopata nafasi kama hizi ni dhahiri kuwa Tanzania inazidi kujulikana.

‘Sometimes watanzania tunasahau kama Mond anavyokula ruti, Idris anavyokula ruti, Vanessa Mdee anavyokula ruti huwa inamaanisha Tanzania imeenda mbali na yoyote kati ya watanzania anakua amefunguliwa ile njia’.-Idris Sultan
‘This is 2017 tukiacha kushushana na kulogana labda tunaweza kuwa mbali sana, na kimoja ambacho tunadharau sana ni Kiingereza na tunakua na maneno kama mbona wachina hawaongei ila wameendelea’Idris Sultan
‘(Niambie vifaa vitano unavyovijua vinavyotengenezwa Tanzania maana hata toothpick tu tunaagiza). WE NEED TO LEARN ENGLISH WE HAVE NO WAY OUT. As for Diamond mi na wewe tunaongea na kuzinguana daily ila hata tutaniane vipi siwezi kusahau kukupa your credit nikaenda kukupea kwenye simu (unaponipigaga mabango) ’-Idris Sultan

Nakupa hapa ili na wewe uache kunipaga hongera kwenye simu 😂 haya great show na Tanzania is well represented ningekuita Simba ila utashindwa kunywa juisi za Azam na ukirudi waelezee kwanini upewe bendera ya kupeperusha we ukashonee sare za madensa wako  #ThatIsKrezi –Idris Sultan 

>>ManyamaJr

1 comment:

Powered by Blogger.