Trending News>>

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 101 & 102 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
"John rafiki yangu, Sheila mke wangu, niwakate kate, kate vipande vigogo vidogo kama nyana. Au mufe kwa bomu hili, litakalo wachangua vipande vidogo vidogo"
Sheila badala ya kujibu, akaangua kilio likubwa kilichonifanya nimtandike ngumi nzito ya shavu, hadi taya ikapinda, huku meno baadhi yakianguka chini.

ENDELEA
"Ahaaaaa fu**"
John alijikuta akitukana kwa kitendo nilicho mfanyia mke wake. Sheila akaendelea kuangua kilio cha majuto sana.
"Nipe kisu"
Pretty akanipatia kisu chenye makali, John akabaki akiwa amenitumbulia mimacho, huku hakiema kwa woga. Nikamkita John kisu cha kwenye paja, la mguu wake wa kulia.
 
"Mamaaaa.."
John alilia kwa uchungu, ulio changanyika na maumivu makali.
"Ahaa kuna kitu nahitaji ukifanye kabla haujakufa"
Nilizungumza huku, nikikizungusha kusu kilicho zama kwenye paja lake, John akazidi kutoa mlio wa machozi.
"Kuna mali zangu, ulizo zichukua wewe na ulivyo mjinga ukaamua kumdhulumu Madam Merry. Sasa nazihitaji zote zirudi kwangu"
 
"Na....ru..disha"
"Sawa kama utazirudisha"
"E...ddy tusa...mehe"
Sheila alizungumza kwa sauti iliyo legea, kutokana na ukosefu wa meno yake mdomoni na kuvunjika kwa taya yake.
"Tena wewe usizungunze. Ni mwanamke gani usiye na huruma katika maisha yangu. Ulipanga kuniua mimi ili muchukue mali za mama yangu. Kwa bahati mbaya ukamuua Fredy. Mtu niliye fanana naye. Leo hii unasema kwamba niwasamehe"
Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama Sheila jinsi anavyo vuja damu.
"Nimezaliwa na roho ya kiatili, na sijawahi kumsamehe mtu abaye kwenda kinyume na mimi."
Nikachukua mkasi mkubwa kiasi. Nikashika kidole kimoja cha John na kukichomeka katikati ya mkasi.
 
"Ngoja ngoja usinikate nikuambie ukweli"
John alizungumza huku akiendelea kulia hadi makamasi yakaanza kumwagika puani mwake.
"Mali zote nilizo zichukua, kuma mtu ndio mmiliki kabisa na mimi ndio nilikua ninamsimamia"
"Nani?"
"Mzee Godwin na.....na yupo Oman, ndipo yalipo makazi yake"
Ikawa ni taarifa nyingine mpya kwani mzee Godwini ninavyo fahamu mimi amefungwa. Ila gereza alilo fungu ndio sikulifahamu.
"Mmmm kwahiyo, hajafumgwa yeye?"
"Haa....hajafumgwa na mtu aliye kua akishirikiana naye ni madam Mery"

Nikakaa kimya huku nikimtazama John usoni mwake. Sikuhitaji kumuonea huruma John hata kidogo. Nikakikata kidole chake kwa kutumia mkasi na lukitenganisha na vidole vinne vilivyo bakia kwenye mkono wake.
"Nahitaji namba za akaunti zako zote za benki"
"Ehee tena ngoja nichukue laptop"
Pretty alizungumza huku akitoka kwenye chumba tulichopo. Ptetty akarudi akiwa na laptop yake.
"Tunaweza kuzihamisha hizo popote pale kwenye akaunti ya benki"
Pretty alizungumza huku akiminya minya batani za laptop yake.
 
"Kwanza una akaunti ngapi?"
"Eheeee?"
"Hujanisikia eheee"
Nikachukua koleo, nikalichomeka kwenye sikio la John, la upande wa kushoto na kuanza kulibana taratibu.
"Nakuambia hiviiii, una akaunti ngapi za benki"
Nilizungumza kwa sauti ya kumnong'oneza John
"Tano tano"
John alijibu kwa sauti ya juu.
"Kumbe unanisikia vuzuri. Ila una ihakika ni tano?"
Nilizungumza huku nikiminya zaidi sikio lake
"Zipo saba, nyimgine ni....ni ni...."
"Ni..ni ni sizihitaji kuzisikia, una akaunti ngapi?"
"Kumi"
Nikajikuta nikicheka kwa maana kili ninavyo zidi kulibana sikio lake ndivyo kila alivyo zidisha kutaja idadi ya akaunti zake za benki.
"Tutajie namba ya akaunti na beki"
John akataja namba ya kwanza, huku akimwagikwa na machozi.
 
"Ni ya benki gani?"
Pretty alimuuliza, huku akiendea kuminya batani za laptop yake.
"Co-operative"
"Ya London?"
"Ndio"
"Yes Eddy, imesoma, tunaomba namba ya siri"
John akataja, Pretty akaiingiza na kusubiria kwa muda kidogo.
"Ohoo My God, Eddy njoo uone"
Nikaliachi sikio la John na kwenda alipo Pretty. Akanionyesha kiasi cha pesa kilichopo kwenye akaunti hiyo. Ambacho dola za limarekani bilioni kumi.
"Eheeee, John mwanangu, kumbe wewe nintajiri hivi. Ukiambiwa utakufa na kuziacha hizi"
   Nilizumgumza huku nikimcheka John, ambaye uhai wake upo mikononi mwangu. Nikamtajia Ptetty namba za akaunti yangu ambayo nahitaji wazihamishe pesa hiyo.
 
"Ohoo wanataja alama ya dole gumba la John ili waweze kudhibitisha kuzihamisha kwenda kwenye akaunti yako"
"Wanataka la upande gani, hilo dolr gumba?"
"Kulia"
Nikachukua mkasi wangu na kumfwata John alipo.
"Nina kazi na kidole chako"
"Eddy kikatie chini chini kidogo ili kifiti hapa"
Pretty aliniambia, John akanitumbulia mimacho akihisi kwamba sinto fanya hilo swala. Nikalikamata dole gumba la kulia na kulikata kwa nguvu. Sheila akatoa ukelele, kama yeye ndio aliye katwa.
 
"Kinacho kuliza na wewe? Nahisi hili tukio si geni kwako, kwani Derick yule malaya wako naye alikufa kama huyu"
  Nikakichukua kidole cha John na kwenda sehemu alipo kaa, Pretty.
"Kisuuze kwanza bwana, si unaona kimejaa damu"
Nikakisuuza vizuri kidole cha John kwa kutumia maji, nikampa Pretty akakiweka kwenye kifaa kingine, alicho chomeka waya wake kwenye laptop. Mwanga mwekundu ukapita kwenye kidole cha John,
"Hapo kinafanyaje?"
"Nina kiscan. Yes kimesoma"
Pretty akanionyesha, kidole kimefanana na alama ya dole gumba iliyopo kwenye benki hiyo.
"Sasa pesa hapa tunaweza kuihamisha"

Pretty akaanza kufanya, kazi ya kuhamisha pesa hiyo kwenye akaunti yangu.
"Asilimia zinakwenda taratibu?"
"Kwa nini?"
"Pesa nyingii hii"
Kama robo saa, pesa, yote ikawa imekamilika luhamishiwa kwenye akaunti yangu. John akaendelea kututajia akaunti zote anazo zimiliki na zote zina pesa nyinhi tu. Pesa nyingine nilimpa ruhusa, Pretty akazihamishia kwenye akauti yake.

Hadi inafika majira ya saa kumi jioni, tukawa tumelikamilisha zoezi zima la kumfilisi John kwenye maakaunti yake ya benki.
"Vifo vyenu nahitaji viwe vya taratibu mno"
Nilizungumza huku nikinywa juisi, aliyo nipa Pretty, hii ni baada ya kukaa kwa muda mrefu pasipo kula chocho.
"Eddy nisamehe kaka, kwani haya yote niliyafanya kwa tamaa"
"Ahaaa tamaaa?"
"Pretty ile video ya mauaji ya Victoria iweke mtandaoni, kila mtu ajionee ukatili wa huyu mjinga"
 
"Sawa bosi"
Pretty akamuonyesha John, ile vodeo jinsi alivyo muua Voctoria, John akabaki akitokwa na machozi mengi. Sheila naye akabaki akikodoa mimacho, hata kuzungumza alishindwa kutokana na taya kuvunjika.
"Una jengine la kuzungumza?"
John akatingisja kichwa kwamba hana la kuzungumza. Nikachomoa bastola, kiunoni mwangu. Nikaifunga kiwambo cha kuzuia sauti.
"Yupi awe wa kwanza kufa?"
Hakuna aliye nijibu zaidi ya woye kukaa kimya. Nikampiga John risasi za miguu, kwenye magoti, kisha nikachukua kishoka kidogo cha kukatia nyama. Nikakata viganja vyake vya mikono yote miwili.

  Yote niliyo yafanya Pretty na Sheila waliyashuhudia kwa macho yao mawili. John alilia kwa uchungu mkubwa huku akiniomba nisimuue ila sikumpatia msamaha wa aina yoyote. Nikamgeukia Sheila na kumtazama kwa macho yaloyo jaa chuki na hasira kali. 
 
"Ed.."
Sheila aliniita, kabla hajamaliza kuliita jina langu, nikampiga risasi tano za kifuani mwake, nikachukua bomu, lakutega. Nikaliweka mbele ya John huku nikiwa nimelitega dakika tano lilipuke.
"Kifo hichi ndicho unacho stahili John"
Nikamaliza kumpiga John risasi za miguu yake yote, hadi nilipo hakilisja hatoweza kusimama wala kulishika bomu hilo, kwani hana tena viganja vya mikono.
 
Tukatoka na Pretty hadi nje, Pretty akachukua gari lake jengine na tukaliacha gari tulilo kuja nalo, kuepuka kukamatwa na polisi. Tukaondoka eneo la nyumbani, hatukufika mbali sana nyumba nzima ikalipuka huku John na mwili wa Sheila vikiwa ndani.
"Eddy inabidi ukatubu kwa Mungu wako"
Pretty alizungumza huku akiendelea kuendesha gari kwa kasi. Tukaingia kwenye barabara ile tuliyo pita jana, iliyo nyooka. Tukaingia mjini majira ya saa mbili usiku, ambapo tukaelekea moja kwa moja hotelini.
Nikafika chumbani kwangu na kuchukua kila kilicho changu, nikarudisha funguo kwa wahusika
Nikatoka nje na kumkuta Ptetty akinisubiri ili anisindikize uwanja wa ndege. Nikaingia ndani ya gari na tukaondoka eneo la hotelini.
 
"Eddy kuna kitu nitahitaji nikuambie kabla hukaondoka"
"Kitu gani?"
"Mimi ni mpeleleIi wa kikosi cha CIA, nilipewa zamana ya kukulinda na serikali yangu ya Marekani."
Nikastuka kusikia aliyo niambia Pretty.
"Usistuke kwa maana bado matatizo kwako hayaja kwisha"
"Una maanisha nini?"
"Baba yako, anakutafuta ili akuue"
"Wewe unejuaje?"
"Mim ni mpelezi ni lazima nilihisi hilo. Ninacho kusihi sasa nenda Tanzania na uipeleke mbali familia yako la sivyo watauawa"
  Pretty alizungumza kwa msisitizo mkubwa, ulio ifanya akili yangu kuanza kumfikiria mzee Godwin. Tukafika uwanja wa ndege, kabla ya kushuka, kutoka ndani ya gari akanisogelea na kunibusu mdomoni
 
"Nakitakia safari njema Eddy"
Ptetty alizungumza kwa sauti ya unyonge huku machozi yakimlenga lenga. Nikaupitisha mkono wangu kwa nyuma, nikakiasogeza kichwa chake karibu yangu, tukanyonyana midomo yetu kama dakika tatu na kumuachia, huku akihema kwa pumzi nzito iliyo jaa mahaba.
Nikafungua mlango na kushuka, nikachukua begi langu lililopo kwenye buti. Nikamtazama Pretty aliye kataa kushuka kwenye gari, machozi yakawa yanamtiririka.
"Pretty bye"
Pretty hakunijibu kitu zaidi ya kuendelea kulia kwa uchungu mwingi. Nikaelekea sehemu ya kukatia tiketi kwa bahati nzuri nikapata tiketi moja ya ndege, iliyokua ikiondoka nusu saa badaye. Nikasimama kwenye foleni ya watu wanao kaguliwa na mizigo yao, ili kuelekea kwenye ndege.
 
"Eddy Eddy"
Nikageuka nyuma na kumuona Pretty akija kasi, huku akilia. Ikanibidi nitoke nje ya foleni, Pretty akanirukia na kunikumbatia kwa nguvu. Machozi yakazidi kumtomka
"Eddy usiende popote, ninakupenda sana"
Ptetty alizungumza huku akiendelea kulia, akaniachia na kusimama huku akinitazama.
"JAMANI NINAMPENDA EDDY GODWIN, NAHITAJI ANIOE"
Nilimshangaa Pretty akizungumza kwa sauti kubwa, iliyo wafanya watu wote kututazama. Bila ya aibu Ptetty akanikumbatia na kuanza kuzinyonya lipsi zangu, jambo lililo wafanya watu wote kupiga makofi ya kushangilia
 
    ****SORRY MADA****(102)
   Ikanilazimu kumtoa Pretty kwenye mwili wangu, taratibu.
"Ptetty"
Nilimuuita kwa sauti ya upole, huku nikimtazama machoni mwake.
"Mmmmm, nakupenda sana, ila ninakuomba kitu kimoja tu unisaidie kwa wakati huu"
"Kitu gani?"
"Ninakuomba, uniruhusu nikaiweke familia yangu katika sehemu salama."
"Eddy nimekuzoea sana. Ninakuomba twende wote"
"No no, nitarejea mama, kwa ajili yako, ninakuomba uniruhusu katika hilo."
Pretty akakaa kimya huku akinitazama machoni mwangu, machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake.
"Promise me"(Niahidi)
"Nitarejea mpenzi, kwa ajili yako"
"Kweli?"
"Ndio"
 
Ilinilazimu kutumia akili nyingi na busara kubwa kumdanganya Pretty la sivyo nisinge ondoka na hata ndege niliyo ibahatisha kwa ajili ya usafiri nisinge ipata.
Pretty akanikumbatia tena, akunibusu mdomoni, huku akilia, nikamfuta machozi kwa kutumia viganja vyangu.
"Nitarudi baby"
"Ok, safari njema"
Pretty alizungumza kwa kujikaza, kwa maana uchungu alio kuwa nao ni mkubwa sana
"Kuwa makini, Eddy"
"Na wewe pia"
Pretty akaniruhusu kuondoka, nikapiga hatua za haraka hadi kwenye foleni ya ukaguzi. Nikavua vitu vinavyo hitaji kuvuliwa ikiwemo, mkanda wa suruali, saa ya mkononi, viatu na simu yangu nikawakabidhi. Nikafanikiwa kupita salana kwenye kitengo hicho, nikachukua kila kilocho changu na kwenda kujumuika na wasafiri wengine.
 
Tukaingia ndani ya ndege, huku nikiwa ninafuraha sana, kwani ni muda wa kwenda kumuonyesha mama yangu, familia yangu aliyokua akiikataa kisa wao ni waarabu ambao mara nyingi alidai mke wangu ni gaidi, kumbe Sheila ni gaidi mkubwa aliye kuwa amejificha kwenye familia yake.
Nikakaa kwenye siti yangu, ambapo pembeni nikamkuta mtu akisoma gazeti kubwa, lilolo ificha sura yale huku kichwani mwake akiwa na kofia kubwa.
"Hi...!!"
Nilijipendekeza kusalimia, kwani si uungwana kukaa siti moja na mtu pasipo kusalimiana naye. Akalishusha gazeti lake chini kidogo, ndipo nilipo pata nafasi ya kuiona sura yake vizuri.
Ni mzee wamakamo aliye enda umri kidogo, anaasili ya kiarabu, huku ndevu zake zikiwa za rangi nyeupe.
 
"Hakunijibu kitu zaidi ya kunitazana kwa sekunde kadhaa, kisha akalirudisha gazeti lake usawa ulio kuwepo awali na kuufunika uso wake kabisa.
"Mmmmm"
Niliguna, huku na mimi nikifunga mkanda wa siti niliyo kalia, nikatoa simu yangu na kumpigia Blanka
"Vipo dogo"
"Safi kaka, huku lini?"
"Kama wiki hivi, ndio nitarudi, wapo wapi hao"
"Mlimani city, kuna vitu tumekuja chukua"
"Ahaaa, nyumba mulipata?"
"Ndio, tulipata ya kukodi"
"Poa mida"
"Hutaki kuwasalimia leo?"
"Baadaye nitawasalimia"
Nikakata simu na kuiweka kwenye mfumo wa 'Airplane mode' kisha nikairudisha mfukoni, nikaminya minya batanani za kitv kilichopo mbele yangu, nikaweka filamu ninayo ipenda na kuanza kuitazama, huku nikiwa nimevaa earphone, zinazo tumika kusikilizia sauti ya filamu hiyo, hii nikuepuka kumbuguzi mwenzako uliye kaa naye, huku tukisubiria ndege kuwashwa na kuondoka.
 
   Taratibu mashine, za ndege zikawashwa, tukaashiriwa na muhudumu, wa kike aliyopo ndani ya ndege hii, kupitia vipaza sauti vilivyomo ndani ya ndege kwamba kila mmoja ajifunge mkanda na kutulia kwenye siti yake, kwani ndege muda wowote itaweza kuondoka. Muda mchache baadae ndege ikacha ardi ya nchi ya Brazili, jambo lililo nipa furaha kubwa kwani tukio nililo mfanyia John na mkewe wake, laiti kama ninge kamatwa ningeozea jela, maisha yangu yote
'Asante mungu'
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikijiweka sawa kwenye siti yangu
                  **
   Mzee aliye kaa pembeni yangu, akalikunja gazeti lake kwa haraka. akachunguli nje kwa kupitia kioo kilichopo pembeni yake, kutokana na giza hakuweza kuona chochote, akalifunga dirisha na kukiziba kioo hicho.
 
Akanitazama huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana. Akavua kofia lake ambalo mara nyingi hupendwa kuvaliwa na watu wanao jiita 'Cow boys'(Ng'ombe wa kiume). Akaliweka pembeni huku jasho likianza kumwagika, jambo lililo anza kunipa wasiwasi na mashaka makubwa dhidi yake.
 
Akaanza kuzungumza maneno yakiarabu yaliyo nipa wasiwasi, kwani maneno yake ni kama ya yule mtu aliye jilipua nikiiwa hotelini, nchini Iraque, akapelekea mimi kupelekwa kwenye hospitali, ambayo nilikutana na Phidaya kwa mara yaa kwanza, akiwa kama daktari aliye nitetea kufa na kupona, pale madaktari wezake walipokua wakihitaji kunikata mguu.

Mzee huyo akavua koti la suti yake akabakiwa na shati lililo tuna mbele, kwa haraka nikamshika na kuchana shati lake hadi vifungo vikakatika.
"Bomuuuuuu"
Nilijikuta nikizungumza kwa sauti ya juu, baada ya kukuta bomu linalo kwenda kwa kasi sekunde zake, zinazo onekana kwa rangi nyekundu, alilo lifunga tumboni mwake. Watu wote waliopo siti za mbele wakanyanyuka na kuanza kupiga kelele, huku wengine wakimuita Mungu wao. Nikataka kuondoka mzee akaniwahi kunidaka mkono, kila nilipo jaribu kuondoka, akanishinda nguvu. Nikalishuhudia bomu lilifika kwenye namba za sifuri, likiashiria lipo tayari kwa kulipuka.
"Buuuuuuuuupuuuuuuuuu"
Bomu likalipuka, na kutuchangua sote tuliomo ndani ya ndege
 
             **
  Nikastuka kutoka usingizini, huku nikihema sana, macho yangu yakatua kwenye kiji tv kadogo kalichopo mbele yangu, kikionyesha tukio la filamu hiyo, ikiwa na mlipuko wa bomu, kwenye moja ya kipande chake, niliyo kuwa nikiitazama kabla sijapitiwa na usingizi. Nikavua earphone huku ikinilazimu kumgeukia mzee aliyopo pembeni kwa haraka, nikalivuta gazeti lake alilo kua akiendelea kulisoma na kumfanya astuke huku akinitumbulia mimamcho yamshangao.
 
"What....!!?"(Nini....!!?)
Mzee aliniuliza, huku akiendelea kunitumbulia mimacho, nikampiga kisukusuku cha uso, kilicho mfanya akae kimya, huku damu za puani zikianza kumchuruzika. Nikamfungua vifungo vya shati lake, nikakuta hana kitu chochote alicho kifunga tumboni mwake zaidi ya msalaba mkubwa alio uvaa shingoni na kuning'inia tumboni mwakr, nikakichomoa kitambulisho alicho kichomeka kwenye mfuko wa shati lake.
'Rev: Frank Dismas'
 
Kitambulisho chake kilionyesha ni mchungaji, wa shirika la misaada duniani
"Am sorry"(Nisamehe)
Nilizungumza huku nikimuachia mchungaji huyu, niliye muona kama ni gaidi, aliye jifunga bomu. Hakunijibu chochote zaidi ya kukaa kimya, huku akizifuta damu zake puani kwa kutambaa. Tukio nililo lifanya juu ya huyu mchungaji, halikuonwa na watu wengi, kutokana na wao kalala, kwa uchovu wa safari hii.
  Hamu ya kuendelea kukaa kwenye siti hii, ikanipotea kabisa, kwa maana mchungaji huyu hakuzumgumza chochote na mimi, wala sikujua kama amenisamehe au laa. Akanyanyuka na kuniomba nimpishe, nikafanya hivyo. Akaelekea maeneo ya chooni, huku mara kadhaa akigeuka nyuma na kunitazama mimi, kama mtu mwenye wasiwasi mkubwa na mimi.
 
"Huyu mzee vipi"
Nilizumgumza huku, nikiedelea kumtilia mashaka, moyo wangu nikaulazimisha kumuamini mzee huyu, ila ikakataa kumuamini kabisa. Nikanyanyuka na kuelekea kilipo choo. Kitendo cha kufika mlagoni tu, nikamkuta naye anafungua mlango, akanitazama kwa muda.
"Buuuuupuuuuuuuuu"
Alinisemesha maneno, nisiyo yaelewa huku akitabasamu kidharau. Nikabaki nikimshangaa, kwa jinsi alivyo nifanyia huyu mzee, kwa mara ya kwanza nilimuota ila hii ya pili ni kitu kinacho fanyika kiukweli. Nikamtazama, akielelea kwenye siti, huku nikiendelea kumyafakari mzee huyu maana ya kunifanyia hivyo ni nini, na nikwanni amenifanyia mimi peke yangu.
 
"Chizi nini huyu? au ni kile kisukusuku, nilicho mpiga?"
Nilijisemea mwenyewe huku nikiingia  chooni.
   Nikafungua zipu ya suruali yangu, kwa ajili ya kujisaidia haja ndogo. Kabla sijaanza nikahisi kuna kijimlio kikitokea chini ya sinki la kunawia mikono. Ikanilazimu kusitisha zoezi zima, nililo kua nikihitaji kulifanya, taratibu nikainama na kuchungulia. Nikakuta bomo, lililo tegwa, kama lile nililo mtegeshea John, huku likiwa limebakisha dakika mbili na sekunde kadhaa kabla halijalipuka.
"Mungu wangu"
Nikatoka chooni haraka, kila niliye mtazama ndani ya ndege, amesinzia, huku baadhi wakiwa wanatazama filamu kwenye tv zao. Sikumuona mzee niliyekuwa nimekaa naye kwenye siti moja, kwani siti zetu mbili zote zilikuwa tupu.
"Amekwenda wapi huyu mchungaji?"
Nilizungumza huku nikiendelea kupepesa macho huku na kule.
 
   Kusema kweli, sikuwa na ujuzi wa kutegua mabomu, nilicho kuwa nikikijua katika mabomu ni kutega tu. Nikamuona muhudumu mmoja  mwanadada, akimfunika shuka, mtoto mmoja, aliye lala muda mrefu.
Nikamfwata na kumuomba, anisikilize shida yangu.
"Do you speak English or Swahili?"(Je unazungumza Kingereza au Kiswahili?)
Nilimuuliza dada huyu, huku jasho likinimwagika usoni, Kwani mimi ndio ninafahamu ukweli unao endelea ndani ya ndege hii, iliyo beba watu wengi si chini ya mia mbili na hamsini, huku watoto na wamama wakiwa ni wengi ndani ya ndege, mbaya zaaidi kwa dakika chache kila kitu kitakuwa kimesambaratika hata miili yetu pia.
 
"Kswahili pia nazungumza"
Aliniambia huku akinitazama machoni kwa umakini. Nikamshika mkono hadi nje ya mlango wa kuingilia chooni.
"Ninakuomba unisikilize kwa umakini, kuna bomu humu chooni, na limebakisha dakika kulipuka...."
"Bomuu....Mungu wangu!"
Dada huyu alishangaa huku akinitumbulia mimacho usoni, ilinibidi kumziba mdomo asizungumze kwa sauti kuashiria watu wengine kuanza shida, zitakazo pelekea sote kupotea kwa uzembe wetu.
"Hakuna haja ya kushangaa"
Nikamvuta na kumuingiza chooni, mikamuonyesha bomu lilipo, Sote tukajikuta tunashangaa kutokana bomu hilo limebakisha sekunde hamsini na tisa, kabla halijalipuka na sote hapa hatujui jinsi ya kulitegua, na muhudumu akaanza kulia, akijaribu kunikumbatia kwani mwisho wetu umefika.

==> ITAENDELEA

No comments:

Powered by Blogger.