Trending News>>

Shirika La Ndege La Rwandair Lapokea Ndege Yake Nyingine Mpya Aina Ya Boeng 737-800 Leo

 Baada ya kupokea ndege mpya aina ya Airbus mwezi wa tisa mwaka huu, Shirika la ndege la Rwandair limepokea tena ndege nyingine mpya aina ya Boeing 737-800 kizazi kipya yenye kubeba abiria 154.

Akizungumza kuhusu ndege hiyo, Meneja mkazi wa RwandAir hapa Tanzania, Ibrahim Bukenya amesema kuwa ujio wa ndege hii umetimiza idadi ya ndege 10 zilizonunuliwa na shirika hilo.

Amesema kuwa kuanzia Disemba 8, 2016 shirika hilo litaongeza safari zake mara 14 kwa wiki badala ya sasa mara 11 kutokea Dar es Salaam kuelekea Kigali na kuunganisha Lagos, Accra, Abidjan, Cotonou, Libreville, Brazzaville, Douala, Kamembe, Lusaka, Johannesburg, Bujumbura, Entebbe, Nairobi, Mombasa, Dubai na Juba.

Bukenya ameendelea kusema kuwa Shirika hilo linategemea kuanzisha safari zake za kuelekea Harare, Bombay na London mwanzo mwa mwezi wa kwanza mwaka 2017.

No comments:

Powered by Blogger.