Trending News>>

PSG wamtafuta Neymar kwa euro milioni 222


Neymar
Image copyrightGETTY IMAGES
Image captionNeymar ana mkataba wa kukaa Barcelona hadi 2021

Klabu ya soka ya Paris Saint-Germain imesema kwa sasa lengo lao ni kumnasa mshambuliaji wa Barcelona Neymar Jr soko litakapofunguliwa majira yajayo ya joto.
Mabingwa hao wa Ufaransa wako tayari kuweka mezani dau la euro milioni 222 kwa ajili ya raia huyo wa Brazil, kiasi ambacho kitawafanya wampate kutokana na kipengele cha kumwachilia huru kilichopo kwenye mkataba wake na Barcelona, kwa mujibu wa tovuti ya Goal.com
Goal wameripoti kwamba, vyanzo vya karibu na mchezaji huyo vimethibisha kwamba uhamisho huo ulikaribia kukamilika hadi pale Neymar alipoamua kusaini mkataba mpya na Barcelona.
PSG wanatarajia kurudi tena kwa mchezaji huyo mara baada ya msimu huu kukamilika.
Iwapo juhudi za kumsajili Neymar zitafanikiwa, nyota huyo atakuwa akilipwa mshahara sawa na ule anaolipwa nyota wa Barcelona Lionel Messi.
Mkataba mpya wa Neymar unaomalizika 2021 una thamani ya euro milioni 25 kwa mwaka mbali zaidi na ule wa Messi wenye thamani ya euro milioni 42 kama mshahara wake wa mwaka mzima.
Endapo Neymar atahamia Paris, ataungana na ndugu zake wa Brazil Marquinhos, Lucas Moura pamoja na Thiago Silva kwenye mji huo mkuu wa Ufaransa.

No comments:

Powered by Blogger.