Trending News>>

MNAOWAKATILI WATOTO WA KIKE MUNGU ANAWAONA!!




Wamewakosea nini? Ni dhambi kuzaliwa mwanamke? Nani atawaepusha na kadhia hizi kama sio mimi na wewe? Imetosha!!!! Mimba na ndoa za utotoni zinaepukika chukua hatua kumlinda mtoto wa kike. Ni kama mfungwa anayesubiria kunyongwa ama kuishi kwenye mateso makali yasiyosimulika pale unapozaliwa wa kike katika mkoa wa Mara ama Shinyanga, mikoa hii ndio vinara wa ndoa za utotoni na huku kukisheheni vitendo vya kikatili vya ukeketeji.

siku-ya-mtoto-wa-kike-2 

Leo ni maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambapo kitaifa inaadhimishwa mkoani Shinyanga, huku serikali kupitia kwa Mkurugenzi wa Watoto Magereth Mussai kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akipinga vikali watoto kukoseshwa haki yao ya msingi ya kupata elimu kwa kukatishwa masomo na kuozeshwa katika umri mdogo na kushindwa kufikia ndoto zao.

Kasi ya ndoa na mimba za utotoni inaongezeka kila uchwao huku vyombo vya habari kupitia kwa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) vikiwa mstari wa mbele kuibua madhambi wanayotendewa watoto wa kike ili kukomesha na kutokomeza kabisa ukatili dhidi wa watoto wa kike.

siku-ya-mtoto-wa-kike-1 

Ni dhahiri Mungu anawaona wale wote wanaotekeleza ukatili huu dhidi ya watoto wa kike na siku ya mwisho kila mmoja atatoa hesabu ya matendo yake; bado nguvu inahitajika katika mapambano dhidi ya ndoa na mimba za utotoni sambamba na ukeketaji kwani kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), inakadiriwa katika kipindi cha miaka kumi ijayo wasichana wapatao milioni moja wanatarajiwa kuwa wameolewa katika umri wa chini ya miaka 18 duniani kote.

watoto

 

 

No comments:

Powered by Blogger.