Trending News>>

ACT Wazalendo yaiomba serikali majibu ya maswali haya mawili

ACT Wazalendo yaiomba serikali majibu ya maswali haya mawili

Tokeo la picha la zitto kabwe
Chama cha ACT Wazalendo kimestushwa Na taarifa kwamba Nchi yetu inabadilisha msimamo wake kuhusu Sahara Magharibi. Tumepata Taarifa kwamba Mfalme wa Morocco ataitembelea Tanzania Hivi karibuni Na kusaini mikataba mbalimbali ya biashara Na Nchi yetu Kwa ahadi kwamba Nchi yetu utaiunga mkono Morocco katika kuifukuza Jamhuri ya Sahrawi kutoka Umoja wa Afrika.
Chama chetu kinaomba ufafanuzi wa Wizara ya Mambo ya Nje juu ya masuala yafuatayo:
• Ni kweli msimamo wa Tanzania kuhusu Sahara Magharibi umebadilika?
• Tanzania itaendelea kuitambua Jamhuri ya Sahara Kama dola Huru Na kulinda kiti chake katika AU?
Sisi ACT Wazalendo tunatangaza dhahiri kwamba hatutaunga mkono kuvunjwa Kwa Msingi Mkuu wa Sera ya Mambo ya Nje ya Nchi yetu ya kusimama Na wanyonge.
Iwapo Serikali itathubutu kuipa mgongo Jamhuri ya Sahara, tutahamasisha wanachama wetu Na Watanzania wengine wenye kuheshimu harakati za ukombozi kufanya MAANDAMANO Siku mfalme wa Morocco anaingia Nchini.
Kamati ya Mambo ya Nje ya ACT Wazalendo imeandika barua Kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuomba kikao naye ili kupata ufafanuzi wa kina kuhusu suala la SAHRAWI.
John Patrick Mbozu
Katibu, Kamati ya Mambo ya Nje, ACT Wazalendo

No comments:

Powered by Blogger.