Baba afunguka kuhusu Samatta kwenda Leicester City
ACHANA na habari za La Liga. Straika namba moja wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta anaweza kuwashangaza mashabiki wake kwa kutua Ligi Kuu ya England muda wowote kuanzia sasa.
Baba mzazi wa mchezaji huyo tajiri zaidi nchini, Mzee Ally Samatta amefichua siri kubwa aliyoelezwa na mwanae huyo kuwa yupo katika mipango mizito ya kujiunga na timu mbili za England ambazo ni Leicester City na West Ham United, huku akisisitiza lolote linaweza kutokea.
Samatta mwenye miaka 25, anayekipiga katika kikosi cha KRC Genk cha Ubelgiji, alitua hapo Januari, 2016 akitokea TP Mazembe ya DR CongoAkizungumza na Championi Jumatano, Mzee Samatta alisema kuwa licha ya mtoto wake kudaiwa kutakiwa na Levante, lakini kwa upande wake alimdokeza ana mpango wa kwenda Leicester City kutokana na kushawishiwa na rafiki yake waliocheza wote Genk kabla ya kutimkia timu hiyo, Wilfred Ndindi.
“Kiukweli hizo taarifa nimezisikia kama watu wengine wanavyosema kwamba sijui hao Levante ya Hispania, wengine wanaitaja Borussia Dortmund ya Ujerumani kuwa nao pia wamekuwa wanamuhitaji, lakini mimi nimeongea naye mwenyewe na alichosema ni kwamba kama mimba ndiyo imetunga basi tusubiri tuone kitakachotokea,” alisema Mzee Samatta na kuongeza.
“Uzuri Samatta kuna watu ndiyo wanamsimamia na hata hilo suala la Levante ndiyo maana akasema tusubiri kitakachotokea kwa sababu mwenyewe yupo kwenye mipango ya kwenda England na timu nilizoambiwa ni Leicester na West Ham lakini Leicester ndiyo sana kwa sababu pale kuna rafiki yake kutoka Nigeria, Wilfred Ndidi ambao walicheza pamoja Genk ila amenisisitiza kwamba atakayekuwa na kisu kikali ndiye atakula nyama.”
Mpaka sasa akiwa na Genk, Samatta amecheza jumla ya mechi 54, za Ligi Kuu Ubelgiji pamoja na michezo 12 ya mashindano ya Europa Ligi. Msimu uliopita haukuwa mzuri kwa Samatta kutokana na kusumbuliwa na goti jambo lililomfanya acheze mechi 35, lakini msimu huu yupo fiti na tayari ameanza kazi.

1 comment:
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment