Trending News>>

Trump aitaka Zimbabwe kuacha kutumia Dola ya Marekani

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema utawala wake uko tayari kufanya kazi na Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe lakini amesisitiza kuwa hilo litawezekana iwapo taifa hilo litaacha kuendelea kutumia Dola ya Marekani.

Amelitaka kutotumia dola hiyo na badala yake lianzishe mfumo utakaohakikisha linatumia sarafu yake ya Zimbabwe. Kwa miaka mingi Zimbabwe ilikoma kutumia sarafu yake na kutumia ile ya Marekani hali ambayo ilikosolewa vikali na wanauchumi.

Duru za habari zimenukuu Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika, Don Yamamoto akisema Zimbabwe anapaswa kudhibiti uchumi wake na siyo kuendelea kutegemea sarafu ya nje.

“ Hivi leo hali ya uchumi wa Zimbabwe ni mbaya. Taifa hili linaagiza chakula kutoka nje, taasisi zake za kiuchumi hazipo katika hali nzuri. Wamelazimika kutumia Dola ya Marekani. Hawapaswi kutegemea sarafu ya Marekani au taifa lingine lolote la kigeni. Haya ndiyo mageuzi tunayopenda kuona yakifanyika sasa,” amenukuliwa waziri huyo akisema.

Amesema Marekani iko tayari kusaidia magaeuzi ya kiuchumi na kisiasa nchini Zimbabwe ili kurejesha taifa hilo katika hali yake ya kawaida. Hatua hiyo imekuja huku Rais Mnangagwa akiyataka mataifa ya magharibi kuliondolewa vikwazo taifa lake vilivyowekwa wakati wa utawala wa mtangulizi wake, Robert Mugabe.

No comments:

Powered by Blogger.