Trending News>>

Simba yapania kurudisha heshima

Klabu ambayo imeanzishwa na mtu binafsi ruksa unaweza kuipumzisha mwaka mzima wawe wanakuimbia nyumbani kwako, sawa. Jasho la wananchi tumeliwekea masharti na sisi hatuko peke yetu duniani, tumeiga mifano halisia katika nchi mbalimbali
Simba inataka kufanya kweli kwenye michuano ya Afrika baada ya kushindwa kuliwakilisha taifa kwa misimu minne mfululizo, baada ya ratiba kutolewa na shirikisho la soka Afrika, afisa  habari wa Simba Haji Manara amesema, wanataka kuendeleza rekodi yao katika michuano hiyo kwa sababu kwa kipindi chote ambacho hawajashiriki mashindano ya kimataifa nchi haikuwa na uwakilishi mzuri.
Manara amesema hakuna timu ya kubeza katika soka la sasa hususan timu ambayo imepata uwakilishi katika mashindano ya vilabu Afrika.
“Ratiba tumeipokea na tumeona ratiba ambayo ipo sawa, wengi wanaona kwamba Djibouti ni dhaifu lakini hivyo wanadhani ni ratiba nyepesi kwetu lakini unapozungumzia mpira sasa hivi hakuna timu dhaifu, Djibouti unaweza ukaona ni dhaifu kwa kuangalia FIFA ranking lakini timu ambayo imepata uwakilishi kwenye CAF Confederation hatuwezi kuidharau hata kidogo.”
“Tutaipa umuhimu hiyo mechi na hatuta wadharau na tunaona kama tunaenda kucheza na timu kubwa kwa sababu sisi malengo yetu sio raundi ya kwanza, kwa sasa tunawaangalia Djibouti baada ya hapo Mungu akijalia tukashinda tunaangalia timu inayokuja. Lengo letu ni kufanya vizuri kwa sababu tumepigana kuipata nafasi kwa miaka minne na unajua nchi haikupata uwakilishi mzuri kwa kipindi chote hicho kwa hiyo tunadhani tutaenda kuendeleza rekodi yetu nzuri ya uwakilishi bora kwenye mashindano ya vilabu Afrika.”
“Sasa hivi tunaweka sawa masuala ya kiusajili nadhani tarehe 15 au 16 nitawaita waandishi wa habari kuelezea mipango na mikakati yetu kwa ujumla kuelekea January mpaka mwisho wa msimu huu pamoja na mashindano ya kimataifa.”

No comments:

Powered by Blogger.