Trending News>>

Shibuda amuomba Rais JPM kuvipiga jeki vyama visivyopata ruzuku

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Ada Tadea, John Shibuda, amemuomba Rais John Magufuli kutoa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa visivyopata ruzuku, ili viweze kushiriki katika uchaguzi wa marudio kwenye majimbo matatu unaotarajiwa kufanyika Januari 13,2018.
Shibuda ametoa ombi hilo leo Disemba 18 kwenye Mkutano Mkuu wa tisa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo amesema hadi sasa kuna vyama vya siasa takribani kumi vilivyotangaza kushiriki uchaguzi huo, huku akimuomba Rais Magufuli kukipa kiasi cha milioni 60 chama chake cha Ada Tadea ili kiweze kushiriki uchaguzi wa marudio.
Katika hatua nyingine, Shibuda amevishangaa vyama vya siasa vya upinzani vilivyosusia kushiriki uchaguzi wa marudio pamoja na kutohudhuria kwenye sherehe za kitaifa licha ya kupewa fedha za ruzuku na kuwaita kuwa si wazalendo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo amevipasha vyama vya siasa vilivyotangaza kususia uchaguzi kuwa, uamuzi huo hautawezi kuiondoa CCM madarakani.
“Wanaoshindana na CCM wajue kwamba CCM linatisha tusitumie muda mwingi kuliangusha, na ukitaka kuliangusha ujue uko wapi lisije likakuangusha. Wisi ni watanzania na mama yetu ni Tanzania, mwanasiasa anayeishambulia Tanzania si mzalendo. Tunaoshindana nawaomba tuangalie Tanzania kwanza tuache mchezo wa kususia susia, hatuwezi kuiondoa CCM kwa mchezo huo,” amesema.

No comments:

Powered by Blogger.