Husna, Wolper Wamaliza Bifu Lao!

Jacqueline Wolper.
MASTAA wawili waliokuwa na bifu kwa sababu ya kuchangia bwana Mkongo
ajulikanaye kama Mwami Radjabu, Jacqueline Wolper na Husna Maulid
wamemaliza uhasama kati yao na sasa ni full vicheko.Hali hiyo ilijidhihirisha juzikati kwenye sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Wolper, walipoonekana wakiwa karibu na
Husna Maulid.
“Si unajua Husna alishamwagana na Mwami ambaye alimvisha mpaka pete ya uchumba lakini hawakufanikiwa kufunga ndoa, kwa hiyo walimaliza tofauti zao,” kilisema chanzo.
Baada ya kuona na kupata habari kutoka kwa chanzo, Za Motomoto News
ilimtafuta Husna ambaye awali alikuwa hapendi kabisa kumsikia Wolper ambaye alikiri kumaliza tofauti zao.
“Tulishamaliza tofauti zetu, sina bifu na Wolper maana aliyekuwa anatugombanisha ni mwanaume na sisi ni wanawake hivyo wanawake tujifunze kuwa wanaume ni watu wa kupita tu,” alisema Husna.
No comments:
Post a Comment