Trending News>>

Rais Kenyatta kuapishwa jumanne wiki ijayo


Rais Kenyatta.

Rais Kenyatta sasa anatarajiwa kuapishwa kuwa Rais kwa muhula wa pili baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali kesi ambazo zilikuwa zinapinga ushindi wake katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 Oktoba.

Kifungu 141(1b) cha Katiba ya Kenya kinasema Rais anafaa kuapishwa siku ya saba inayofuata siku ya kutolewa kwa uamuzi wa mahakama wa kuidhinisha uchaguzi iwapo kulikuwa na kesi iliyokuwa imewasilishwa.

Rais, kwa mujibu wa katiba, anafaa kuapishwa hadharani mbele ya Jaji Mkuu au Naibu Jaji Mkuu.

No comments:

Powered by Blogger.