Trending News>>

Nitamtokeaje huyu Msichana?



Inaonesha ni mgeni kaja kutembea kwa dada’ke, hapo alipo mi hua napita tu kama njia ni mtoto mzuri mwenye lordeyes, mweusi, mkarimu, mwenye aibu nyingi sio siri nimemzimikia kwa kweli, tatizo linakuja ni kwamba hatoki kwao wala hana rafiki wa karibu na hapo kwao muda mwingi yupo na family members so nashindwa hata kumchomoa kidogo pembeni naishia tu kumsalimia.
Nje kwao wana genge siku moja nikaplan siku akiwa peke yake nikanunue kitu pale ili nipate angalau dk 5 nimalize kazi, nikapata chance hiyo nikajitia uchizi kwenda kununua kitu chochote cha kutafuna kufika pale nikakutana na maembe mabichi ikabidi ninunue mwanaume nikajikaza nikala embe bichi kama mwanamke mjamzito. Sasa kila nikitaka kuanzisha story wanatokea wateja so akawa busy mpaka namaliza kula lile embe ikabidi nitambae, zimepita kama siku 2 hivi nikitaraji kupata chance kama ile lakini wapi kila nikipita nakuta shari kwao sasa nimeona bora nimuandikie later nimkabidhi pale kiaina alafu atajua mwenyewe.

No comments:

Powered by Blogger.