Trending News>>

Kwa nini Diski Kuu ktk Kompyuta za Windows huitwa Drive ‘C’ na si A au B?

Kama ni mtumiaji wa kompyuta zinazotumia Windows utagundua ya kwamba mara zote diski uhifadhi kuu (hard drive) katika kompyuta yako hupewa jina la Drive C. 
Floppy Diski
Ukiwa unapakua (install) programu ya Windows kwenye kompyuta yako hakuna kabisa uwezo wa kuipa jina la A wala B, na diski zingine utakazochomeka n.k huchukua herufi nyinginezo lakini kamwe si A wala B.
Sababu – Kihistoria…
Kabla ya teknlojia za ‘hard disk’ kuja kompyuta miaka ya zamani zilikuwa zinakuja na Floppy Disk. 
Muonekano wa kompyuta ya zamani, ikiwa ina maeneo mawili kwa ajili ya Floppy Diski
Eneo moja, A: lilitumika kuweka Floppy Drive ambayo ndio ilikuwa na programu endeshaji (OS) ya kompyuta na wakati mwingine nafasi ya pili kwa wenye uwezo mkubwa wa pesa basi walikuwa wanatumia kusomea floppy diski ya pili; hii ilihusisha kutumia programu mbalimbali na kadhalika.
Na hiyo historia ya Drive A na B. Ni kutokana na hivi ndio basi ata pale ambapo teknolojia ya harddisk, ujazo mkubwa zaidi ulipokuja ukapewa eneo la Drive C. 
Drive D huchukuliwa na mfumo wa kusoma CD/DVD.
Muonekano wa floppy diski ikiwa imechomekwa kwa kutumia ‘adaptor’ ya kisasa kwa ajili ya kusomea Floppy Diski
Je ni muhimu sana hali kuendelea hivi?
Ndio, kulazimisha diski yenye programu endeshaji ya Windows kuwa A kunaweza leta ugumu mkubwa kwa kompyuta hiyo kuweza kufanyakazi bila matatizo.
Mfumo mzima wa Windows wa sasa umejengwa katika kuelewa ya kwamba programu endeshaji hiyo huwa inakaa kwenye Drive C, waliojaribu kuweka kwenye A au B kiulazima wamejikuta wakipata tabu.
Inasemekana kutokana na kufahamu ya kwamba teknolojia za uhifadhi data za floppy diski kuwa za kizamani basi ata kompyuta na programu endeshaji huwa zinasoma disk A au B kwa uangalifu sana kama zimechomekwa. Hii ni kutokana na kwamba teknolojia hizo za kizamani zina ubora mdogo na hivyo zinaweza ruhusu virusi kushambulia kompyuta kwa urahisi zaidi.
Muonekano wa Floppy Diski za ukubwa mbalimbali, ya kwanza kushoto ilikuwa inatumika baadhi ya sehemu tuu (makampuni n.k). Ya katikati na kulia ndio zilikuwa zinatumika zaidi.
Je wewe ulitumia kompyuta kipindi ambacho Floppy Diski zilikuwa bado kwenye utumiaji sana au ndio umefahamu kuhusu uwepo wake?
Chanzo: Superuser.com na vyanzo mbalimbali
Tazama video Mtoto amvua kofia
 Papa Francis

No comments:

Powered by Blogger.