Trending News>>

Kama Wewe Ni Mwanaume Basi Hii Inakuhusu. Wanaume Tu Please..!



Mwanaume hahitaji Mwanamke mwenye Sura nzuri kama Miss Utalii na Makalio yanayoweweseka akitembea kama mshumaa uliopulizwa na upepo wa bahari ya Hindi. Hizi ni sifa za muda kwa ajili ya tamaa ya macho na ngono.

KUNA MAISHA ZAIDI YA KUWA NA SURA NZAURI NA KUFANYA MAPENZI
Ndio maana utashangaa Mtu amedate mademu 20 wakali kinoma wenye wezere kama wamejiumba lakini anaoa demu wa ‘kawaidaaaa’ mwenye sura kama amepiga chafya isiyotarajiwa halafu unaanza kujiuliza huyu Kaka amekosa nini..Hajakosa kitu…amevumbua dhahabu.Mwanaume anahitaji Mwanamke MSAIDIZI…MSHAURI…MBEMBELEZAJI…MTIA MOYO…MWENYE MAONO….Sio Mwanamke anajua Club zote mpya ilizofunguliwa Wiki hii lakini hana taarifa kama kuna Plot zinauzwa Madale ili amshauri mmewe ku-acquire Land.
Utashangaa na mkalio wako kama dansa wa Baikoko umetemwa na anaolewa bishosti hajawahi kuvaa kipedo tangu azaliwe,anavaa charanga.
Kama unadhani Shepu ni mali nenda kaombe kazi Twanga Pepeta…Tutaendelea kuoa vituko kwa sababu Vina Akili na Vinajiheshimu na wewe utaendelea kualikwa kwenye harusi kama Mtazamaji kwa sababu HUOLEKI.

No comments:

Powered by Blogger.