Trending News>>

Usaliti wa Manchester United ulimfanya “Dinho” aende Barca

Hakika Ronaldinho Gaucho ni mchezaji ambaye kila klabu inatamani angekuwa mchezaji wao kutokana na ubora aliokuwa nao Mbrazil huyo katika kipindi chake.
Mwaka 2003 inasemekana Joan Laporta ambaye ni mwanasiasa nchini Hispania lakini pia alikuwa raisi wa klabu ya Barcelona alimsaini Ronaldinho baada ya Manchester United kumzunguka.
Ilikuwa hivi, klabu ya Manchester United walikubaliana na Laporta kwamba akishinda uchaguzi Barcelona baasi watawauzia David Beckham aliyekuwa katika kiwango kizuri.
“Ilikuwa tumchukue Beckham,Ronaldinho au Henry na United wakatuambia watatupa Beckham  lakini hawakufanya hivyo wakatuzunguka wakamuuza Real Madrid” alisema Laporta.
Kumbuka wakati Barcelona wanamtaka David Beckham na kuahidiwa kuuziwa na United, Manchester United nao kipindi hicho walikuwa wakihitaji kumsajili Ronaldinho ambaye kipindi hicho alikuwa PSG.
Manchester United tayari walishatuma ofa kwenda PSG na ilionekana wanakwenda kumchukua Ronaldinho lakini Barcelona waliamua kulipiza walichofanyiwa na Manchester United kwa Beckham.
Barcelona waliamua kutuma ofa kubwa zaidi kwa klabu ya PSG ambayo kwa haraka haraka ilikubaliwa na wakamnunua Ronalinho huku United wakibaki wanashangaa shangaa.
Rinaldinho alipojunga na Barcelona ndio jina lake lilizidi kuwa kubwa na baada ya United kushindwa kufanya usajili huo walihamia kwa Cristiano Ronaldo ambaye naye alifanya vizuri klabuni hapo.

No comments:

Powered by Blogger.