Trending News>>

Unaambiwa Messi alianza Mapenzi akiwa na Miaka 5



Nyota wa kandanda duniani Lionel Messi atafunga pingu za maisha na mpenzi wake wa tangu utotoni katika mji wake wa kuzaliwa nchini Argentina baadaye leo.
Messi, 30, alikutana na mkewe alipokuwa na miaka mitano pekee.
Ni binamuye rafiki yake wa karibu, Lucas Scaglia, ambaye pia ni mchezaji wa kulipwa
Messi alikubali ofa ya kuichezea Barcelona alipokuwa na miaka 13, kwa sharti kwamba wangekuwa wakilipia matibabu yake ya upungufu wa homoni ya ukuaji mwilini.
Amezungumzia changamoto alizokumbana nazo alipolazimika kuwaacha wapendwa wake na klabu yake ya zamani.
Wawili hao, ambao sasa huishi Barcelona, wana wana wawili wa kiume.
Mwezi Mei, rufaa yake dhidi ya kifungo cha miezi 21 jela kwa kukwepa kulipa kodi nchini Uhispania ilikataliwa.
Hata hivyo huenda asiende jela kwani kifungo hicho kinaweza kutumikiwa nje au afidie kwa kulipa faini.

No comments:

Powered by Blogger.