Trending News>>

Kama ulichukuliwa mifugo yako na serikali, fuata utaratibu huu kurejeshewa


Serikali ya Mapinduzi zanizbar imesema wanyama wote waliokamatwa  na serikali   Mei mwaka jana  kwa  lengo la kuimarisha  usafi wa mji ,usalama barabarani  na  kuweka mandhari mazuri  yenye kuvutia wanyama hao watarejeshewa wenyewe kwa utaratibu maalum.
Akijibu swali  la msingi lililoulizwa na Mwakilishi wa Jimbo la Paje Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalumu za SMZ  Haji Omar Kheri amesema utaratibu wa  kuwapata tena wanyama hao  kwa wamiliki wa mifugo hiyo ni kuchukua  barua katika Shehia anayofugwa mnyama husika na kuiwasilisha  barua hiyo  ya utambuzi katika  Manispaa yao
Hata hivyo Haji amesema lazima mfugaji alipie gharama za utunzaji wa wanyama  hao kwa kipindi chote  alichokaa mnyama  katika  hifadhi  ya  serikali  na atakabidhiwa  mnyama wake akiwa amewekwa  alama maalum kwa lengo la udhitibi wa kurudi tena kuwaweka  wanyama hao katika maeneo yasiyoruhusiwa kufuga.
Aidha amefafanua kuwa endapo  mnyama huyo  aliyeekewa  alama atakamatwa tena katika maeneo yasiyoruhusiwa mnyama huyo atakuwa mali ya Serikali  na taratibu  husika za kuuzwa zitafuatwa.
Powered by Blogger.