Trending News>>

SIMULIZI :: Jini Mahabati Sehemu ya Sita (Kwa wenye miaka 18+)


 
SIMULIZI : JINI MAHABATI
SEHEMU YA SITA
MTUNZI: MANYAMASON
AGE: 18+
Radhia naye alishangaa kile kitu kilichokuwa kinamtekenya tekenya kwenye nyeti zake kilitulia ghafla na mshawasha wote wa kufanya mapenzi ulimwisha wote. Akajinyanyua pale kiatandani akakimbilia bafuni kwenda kuoga. Alivyotoka alimkta Juma ameshaondoka.
“Kumbe na mbwembwe zote zile ni hanisi” aliwaza Radhia huku akipanda kitandani na kulala. Kumbe lile pepo la huba linalomtia stimu Radhia lilifukuzwa na harufu ya bangi ya kijana huyo. Na hili kumkomesha lilimpiga kombora hilo maana hawapatani kabisa na harufu ya bangi. Kwa hiyo ile shoto ya mkono na kulala kwa mtarimo wa Juma ilikuwa ni nguvu za kijini za mzimu wa Barike.
***************************
Siku iliyofuata Radhia alienda chuoni huku akiwa na mawazo mazito sana hasijue ni nini hasa kilichomtokea jana usiku au ile nyumba ina mambo ya kishirikina ni maswali ambayo alikuwa akijiuliza Radhia siku nzima bila kupata majibu ya maana.
Akiwa darasani huku akiwa amebaki mwenyewe na mwalimu ameshafundisha na wanafunzi wametoka kupisha wengine alisikia mtu akimgusa mabegani. Akageuka kwa hasira ya kutaka kujua ni nani aliyemgusa na kumuondoa kwenye tafakari nzito ya juu ya nini kilichotokea juzi na jana na kusababisha kupoteza uwanamwali wake alioutunza mpaka akafikisha miaka 21.
Kuangalia alikutana na sura ya Tariq mwanaume aliyekutana naye siku ile akienda kufanya usahili na pia mwanaume aliyemwota kuwa umempeleka ujinini. Ilibidi aoneshe tabasamu zito kuonesha kuwa amemkumbuka. Wakasalimiana na kisha wakaondoka kuwapisha wanafunzi wengine.
Tariq alifurahi sana kugundua kuwa kumbe walikuwa wakisoma darasa moja na binti huyo mrembo. Basi urafiki wao ukawa umeanzia hapo na walipozoeana vya kutosha Tariq hakuacha kujaribu bahati yake ya kumtongoza binti huyo. Lakini Radhia hakuwa tayari kukurupuka na kumkubalia..
***********************
Ni wiki ya tatu sasa tangia ile ndoto imtokee Radhia na yeye aliendelea na maisha yake ya kawaida. Kila siku alikuwa akisumbuliwa na wanaume wakimtaka kimapenzi hasa wababa watu wazima wenye wake na watoto.
Uzuri wake na muonekano wake machoni pa wanaume ulizidi kuwa kivutio na macho yake ya mlegezo yalizidi kuwa silaha tosha ya kuwashawishi wanaume wamtake.
Hamu ya yeye kufanya mapenzi kila siku ilizidi kuongezeka na kuna wakati alihisi kupata muwasho wa huba katika sehemu zake za siri.
“Yaani sijui ni kwa nini  hizi nyeti zangu kila ikifika usiku zinaanza kunitekenye tekenye” hayo ni baadhi ya maswali ambayo yaliyokuwa yakimtatiza Radhia kila siku iendayo kwa Mungu. Akawa anajaribu kumuuliza rafiki yake wa kike kwa jina Zuwena ambaye vyumba vyao vilikuwa vimeongozana juu ya hali hiyo.
Lakini hata rafiki yake alishangaa kusikia eti kuna kitu huwa kinamtekenya tekenya na kumpandisha mshawasha wa kufanya mapenzi. Zuwena alimshauri kama ni hivyo basi atafute mwanume mmoja ambaye atakuwa anamsaidia kumsugua kila hali hiyo inapotokea.
Au pia akionahali inazidi kuwa mbaya siku hadi siku basi waende kwa madaktari au hata kwa viongozi wa dini maana kua kila dalili ya kuwa Radhia alikuwa na pepo la jinni mahabati.
Siku zilizidi kuyoyoma huku Radhia akizidi kuwa gumzo hapo chuoni. Sio wanafunzi sio walimu sio wafanyakazi wakawaida wote walikuwa wakimtamani na kumtaka kimapenzi. Mida ya jioni Radhia alikuwa akipenda sana kwenda uwanjani kufanya mazoezi ya mpira wa Vollyball.
Alikuwa kivutio sana hasa kutokana na staili ya nguo zake za mazoezi ambazo zilikuwa zikionesha mautamu yake. Hali hiyo ilimfanya mwalimu wa michezo kujikuta akishindwa kuvumilia kila alipajaribu kumuangalia bint huyo machoni aliona vitu kama vikopa kopa vikimzunguka.
Basi siku moja mara baada ya mazoezi alijaribu kuongea na binti huyo kiutu uzima. Alimwambia kuna jambo anataka kuongea naye hivyo kama hatojali basi waonane jioni jiooni kwa ajili ya chakula cha usiku. Basi Radhia hakukataa, alikubali out hiyo na hivi ilikuwa ni wikiend aliona hiyo ni nafasi nzuri pia kwake kureflesh mind.
Mwalimu huyo akajikaza na kumpleka out mjini. Alifanya hivyo ili kuepusha macho ya wanafunzi na watu wengine ukizingatia pia na yeye ana mke na watoto.
Walifika mahali wakakaa na baaada ya chakula mwalimu hakusita kueleza ya moyoni. “Ujue Radhia kiukweli mimi nakupenda sana na nimevumilia nimeshindwa nimeonealea leo bora nikwambie tu ukweli ili kama utaamua kunikubalia au kunikatalia basi itakuwa nimejaribu kukueleza hisia zangu”.
Razia alinyamaza kimya huku akifikiria jibu la kumpa. Alimwangalia usoni kwa jicho la mahaba kisha akatabasamu. Kile kitu kinachomsumbauaga kwenye nyeti zake kikaanza tena kumtekenyetekenya na kujikuta akipata stimu za kufanya mapenzi.
“Sijui hata ni kwambiaje” alisema Radhia huku akimwangalia usoni mwalimu huyo. “Sema tu chochote usiogope” alisisitiza Mwalimu hukua akiona vitu vya ajabu ajabu kwenye macho ya binti huyo.
“Kwanza mwalimu wewe si una mke na mtoto juu.?” Aliuliza Radhia, Mwalimu akajibu ndio. “Sasa kwa nini unataka na mimi niwe mpenzi wako”. “Hata miki sielwei yaani nimetokea kukupenda ghafla” alisema mwalimu huyo dhairi bila kificho.
**ITAENDELEA*💋💋💋

No comments:

Powered by Blogger.