Trending News>>

RC Gambo: Tutawadhibiti Wote Wanaoingiza Siasa Misibani

Mkuu wa Arusha Mrisho Gambo amesema serikali itaendelea kuwathibiti watu wote watakaotaka kuingiza siasa kwenye majanga mbalimbali hasa la vifo vya wanafunzi wa Lucky Vicent na kuwataka watu kufuata utaratibu na maelekezo yanayotolewa na serikali.

Mkuu wa mkoa huyo alisema hayo jana wakati anapokea misaada inayoendelea kutolewa na wadau mbalimbali na kuwataka wananchi na taasisi zinazoendelea kutoa rambirambi kwa familia za wanafunzi waliofariki kufuata taratibu zilizowekwa ili kuepusha migongano isiyo ya lazima.

Mbali na hilo Gambo alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwadhibiti wote watakaotaka kuingiza siasa kwenye majanga likiwemo la vifo vya wanafunzi na amesisitiza umuhimu wa kila mmoja kufuata sheria, taratibu na maelekezo yanayotolewa na serikali.


No comments:

Powered by Blogger.