Trending News>>

Mwingine kutoka Azam, ataka asajiliwe Simba

 
KIUNGO wa ulinzi wa kimataifa wa Burundi, Youssouf Ndikumana amesema kwamba yuko tayari kujiunga na washindi wa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC), Simba SC iwapo watafika bei yake.
Akizungumza jana mjini Dodoma, mchezaji huyo wa Mbao FC ya Mwanza alisema kwamba kwake anaangalia maslahi na kama Simba wataweza kutoa kiwango cha fedha anachotaka atajiunga nao.
Youssouf Ndikumana (kulia) katika mahojiano na mwandishi wa habari, Saada Akida jana mjini Dodoma 
"Mimi nipo tayari kujiunga Simba au timu yoyote kati ya hizo zinazotajwa zinanitaka, kikubwa ninaangalia maslahi," alisema.
Ndikumana alicheza vizuri jana katika fainali ya ASFC, ingawa Mbao FC ililala 2-1 mbele ya Simba SC Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Na wakati tayari kuna tetesi za mchezaji huyo kutakiwa na Simba SC, naye amesema yuko tayari kwenda kuungana na Mrundi mwenzake, mshambuliaji Laudit Mavugo...

No comments:

Powered by Blogger.