Trending News>>

MICHEZO:Ernesto Valvarde ateuliwa kuwa kocha mpya Barca, ni nani huyu?


Ernesto ni mzaliwa wa nchini Hispania ambako alizaliwa miaka 53 iliyopita nchini Hispania na amewahi kuichezea timu yake ya taifa huku pia akipita katika vilabu mbalimbali nchini Hispania.
Ernesto Valverde amevichezea vilabu vya Alaves, Sestao, Espanyol,Atletic Bilbao lakini pia alikuwepo katika kikosi cha Barcelona kilichoshinda kombe la Cup Winners Cup na Copa Del Rey chini ya Johan Cruyf.
Mwaka 1997 ndipo Valverde aliamua kuacha kucheza soka na kuanza kujihusisha na masula ya soka ambapo alifundisha timu kama vile Espanyol,Olympiakos,Villareal,Valencia na hatimaye Bilbao.
Uwezo wa Ernesto Valrade ulionekana mkubwa sana haswa walipochukua kombe la Super Cup mwaka 2014 baada ya kuifunga Barcelona mabao 4 kwa nunge hapo ndipo alianza kufahamika sana.
Lakini pia Valvarde sio mgeni sana wa makombe kwani alipokuwa akiinoa Olympiakos alifanikiwa kubeba makombe matano ya michuano mbali mbali nchini Ugiriki.
Valvarde anakwenda kuchukua kazi ya Luis Enrique aliyeamua kustaafu, lakini atakuwa na kibarua kigumu kuirudishia Barca ubingwa wa La Liga na Champions league ambayo yote msimu huu wameikosa.

No comments:

Powered by Blogger.