Trending News>>

Arsenal wanyakua Ubingwa wa kombe la FA

Wachezaji wa Arsenal wakifurahia na Kombe lao la FA England baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Chelsea Uwanja wa Wembley leo. Mabao ya Arsenal yamefungwa na Alexis Sanchez dakika ya nne na Aaron Ramsey dakika ya 79, wakati la Chelsea limefungwa na Diego Costa dakika ya 76. Chelsea ilimaliza pungufu baada ya Victor Moses kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano kwa kujiangusha kwenye boksi dakika ya 68

No comments:

Powered by Blogger.