Trending News>>

Wananchi 21 wafikishwa mahakamani kwa kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi.


Jumla ya watuhumiwa 21 akiwemo mwanamke mmoja wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Chunya kwa kuhusika na vurugu zilizotokana na wananchi wilayani humo kuvamia kituo cha polisi kwa lengo la kuwatoa watuhumiwa wa mauaji ili kuwaadhibu.

Watu hao waliofikishwa mahakamani ni sehemu ya watuhumiwa 41 waliokamatwa, kati yao wanaume wakiwa 34 na wanaweke 7 baada ya vurugu zilizotokea jana na kusabababisha jumla ya watu 7 kujeruhiwa wakiwemo askari polisi wanne, na wananchi watatu huku mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la AMOKE MBILINYI (25) akifariki dunia.

Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya imeeleza kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 18.12.2016 majira ya saa 11:45 asubuhi katika Kituo cha Polisi Makongolosi kilichopo Kata ya Makongolisi, Wilayani Chunya ambapo kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi walivamia kituo hicho cha Polisi na kufanya fujo kwa kuwarushia  mawe hovyo askari.

Kwa mujibu wa jeshi hilo, lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kuwatoa watuhumiwa wawili waliofahamika kwa majina ya 1. ERASTO ROBERT, mkazi wa Kilombero na 2. BASI LINUS mkazi wa Makongolosi waliokuwa wanakabiliwa na kosa la mauaji kwa lengo la kuwatoa nje na kuwauawa kwa kuwachoma moto. 

Aidha wananchi hao walifunga barabara ya Chunya/Makongolosi kwa kuweka mawe makubwa na magogo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa wa watumiaji wengine wa barabara hiyo.

Jeshi hilo limesema thamani ya uharibifu bado kufahamika na hali imerejea kuwa shwari

Awali mnamo tarehe 11.12.2016 majira ya saa 23:20 katika Kitongoji cha Manyanya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JACOB BROWN Mkazi wa Manyanya alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa peke yake shambani kwake na kuuawa ambapo Polisi walifanya msako na kuwakamata watu hao wawili kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.

No comments:

Powered by Blogger.