Trending News>>

VIDEO:Muonekano wa Ndani wa Ndege Boeng 787 Dreamliner Ambayo Serikali Itanunua


Jana Desemba 5, 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Masoko ya Afrika wa Kampuni ya utengenezaji wa ndege ya Boeing yenye makao yake nchini Marekani Bw. Jim Deboo ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kununua ndege kubwa kutoka kampuni hiyo.

Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt. Leonard Chamriho na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James. Baada ya Mazungumzo hayo Rais Magufuli alisema Serikali yake ya Awamu ya Tano imedhamiria kununua ndege nyingine nne zikiwemo ndege kubwa 3 ambazo zitasaidia kuinua uchumi wa nchi kwa kuwezesha watalii kuja hapa nchini moja kwa moja kutoka nchi zao.

Moja ya ndege ambayo serikali imedhamiria kununua inayotarajiwa kuwasili nchini Juni 2018 ni Boeing 787 Dremaliner. Ndege hii ni ya kisasa ambapo ndege ya kwanza ya aina hii ilianza kuruka mwaka 2009 ambapo inauwezo wa kwenye maili 567 (km 912.5) kwa saa moja.

Hapa chini ni video kutoka Shirika la Ndege la Uingereza wakikuonyesha namna ndege hiyo ilivyo pamoja na ubora wake.

TAZAMA VIDEO:

No comments:

Powered by Blogger.