Trending News>>

STORI FUPI YA MAHABATI.


Alikuwa ni rita niliyempenda zaidi pale kazini kwetu , kazi yake sikujua ni nini haswa , lakini nilimwona mara kwa mara akipita huku na kule katika shuguli , mimi kazi yangu ilikuwa ni nyingine kabisa .

Kampuni yetu ilikuwa kubwa na wafanya kazi wengi , ilikuwa sio rahisi kujua watu wote koz wengine wako idara zingine na shuguli zao ni zingine , ndio kama rita sikujua yeye kazi yake wala yuko idara gani .



Lakini alikuwa akipita idara yetu , nikikaa pale katika computer huwa namwona akipita na kuchugulia wakati mwingine anaongea na kiongozi wa idara yetu kisha anaondoka , kweli nilimpenda , siri ilikuwa ni rohoni mwangu .

Kwanza nilivutiwa na sauti yake alivyokuwa anaongea upole na taratibu , ngozi yake nyeupe laini sio ya mkorogo , nilivutiwa na macho yake , nywele zake na mwisho kabisa kuliko zote ni miguu yake , vile vimini nilinichanganya kwa hakika .

Wakati mwingine nilihisi anakuja kwangu labda kunisalimia hivi au kuniuliza kitu Fulani lakini wapi , hata salamu hatowi , nilitafuta contact zake mpaka nikachoka , niliwauliza wafanya kazi wengine walikataa kunipa .

Nilihisi nao wanampenda ndio maana hawataki kunipa contact zake , pia ni mimi mwenyewe nilikuwa ni mtu wa aibu sana , sidhubutu kuongea na mwanamke haswa yeye anayevutia , niliendelea kuvumilia tu .

Siku moja asubuhi , alikuja chumbani kwangu kule kazini , nilikuwa nimekaa mwenyewe ,tu , sikumbuki alikuja kutazama nini , ila alikuja mpaka kule ninapokaa , alipofika nilisimama na kumshika mkono , nilimweleza kwamba nampenda sana .

Hakuamini , aliomba nimnongoneze , nikafanya hivyo , kisha akani hug , nami nilimpiga busu na mdogo tukashikana mikono mpaka mlangoni wakati anatoka nilimwomba tuonane jioni ya siku hiyo kwa maongezi , alikubali kwa furaha .

Nilihisi roho yangu imeingia dhahabu , nilijiona kweli mimi ni mwanajeshi wa mapenzi ,nikaanza kupanga mambo ya jioni , siku hiyo nzima sikufanya kazi nilikuwa na furaha ya kukutana na rita jioni hiyo mambo poa .

Jioni ilifika , rita akanikumbuka alinipitia chumbani kwangu , tulianza safari ya kwenda sehemu Fulani inaitwa sunrise , tulipanda taxi mpaka kule , tulipofika kule tulikaa chini ya mchanga huku tukiongea na tabasamu kwa mbali .

Hapo sunrise kukawa na speaker kubwa tulisikia sauti mpaka kule mchangani , muda huo ilikuwa ni saa 12 jioni , nyimbo iliyokuwa inapigwa ni butterflies ya Michael Jackson , maneno ya nyimbo ile ni matamu yaliendana na wakati ule .

Nyimbo ile iliendana na wakati wetu pale , wote tulilala mchangani tukipigana mabusu , kuchezeana miguu na kutekenyana , taratibu , nilikuwa nimefunga tai wakati wote huo alinivua tai yangu , wakati tukiendelea na mambo mengine .

Aliniambia ananipenda sana kwa mara ya kwanza , hapo moyo ulienda mbio sana , nami nilimwambia pia jinsi nilivyokuwa najisikia siku zote anakuja katika office yetu , tuliongea kwa muda kisha tukasimama kurudi zetu ukumbi mkuu .

Njiani katika mchanga tulikutana na vijana 3 , hao vijana walitusimamisha walikuwa wamevaa jeans wote , mmoja nilimwona na kitu kama bisi bisi hivi , mimi nilimshika rita mkono kumwamuru asijibu chochote tuendelee kwenda zetu .

Ghafla upande wa kulia walitokea vijana wengine 2 wakawa wanakuja kwa kasi kutuvamia , yule mmoja mwenye bisi bisi akachomoa ile bisi bisi yake alitaka amchome nayo rita , ilibidi nimpige ngwala rita adondoke chini , alipofika chini hiyo bisi bisi ilipita juu .

Nikainama chini , kubeba mchanga na kumwagia machoni , hapo alipofuka macho kwa muda , hakuweza kuona vizuri alianza kupiga kelele , wenzake walikuwa na mashaka kuhusu kuendelea na hiyo kasheshe .

Nilimbeba rita wangu , kuendelea na safari , tulipofika karibu na mwanga jamaa mwingine alikuwa na kisu , kwa kunutsukiza ,alirusha kisu kutokea nyuma , mimi na rita tulijidondosha kwa mbele , kukwepa paaa tulidondoka .

Nikawa chini , jamaa akaona ameshanipata nimedondoka , aliruka juu , ili anikanyage na viatu vyake , wakati anajiandaa kuruka nilimpiga mguu mmoja wa kushoto , kabla ya kudondoka chini , nilidaka mguu mwingine kwahiyo mguu mmoja juu mwingine nimeushika .

Niliugeuza na kuutengua , kisha nikachukuwa kisu na kumchomeka mwenyewe shingoni .Mimi na rita tulinyanyuka na kuendelea na safari yetu kurudi nyumbani .

Tulirudi nyumbani na maisha yalikuwa poa tu .

Kesho yake kazini , rita alikuwa akiwahadithia wenzake mambo yalivyokuwa

Kwaheri

No comments:

Powered by Blogger.