Trending News>>

MISS Tanzania wa Mwaka Huu Sio Mtu wa Mchezo Mchezo..Ona Alichowafanyia Wazungu na Huu Wimbo wa Darasa


Miss Tanzania 2016, Diana Edward ameendelea kuonyesha mapenzi yake ya kuendelea kuutangaza muziki wa Tanzania kwenye shindalo la Miss Wolrd linalofanyika nchini Marekani.

Mrembo huyo amepost kipande cha video kwenye mtandao wa Instagram akiwa na mamiss wengine wawili huku wakicheza wimbo wa ‘Muziki’ wa Darassa.

Siku chache zilizopita kupitia mtandao huo, Diana alipost kipande cha video kinamuonesha akiwa na Miss Hondurus, Kerelyne Campigoti Webster na Miss Mexico, Ana Girault wakiucheza wimbo wa Man Fongo, Hainaga Ushemeji.

Kwa sasa mrembo huyo amefanikiwa kuingia fainali ya shindano la Beauty With A Purpose ambalo ni sehemu ya mashindano mbalimbali kwenye Miss World ambalo fainali zake zitafanyika Disemba 18.

VIDEO:

No comments:

Powered by Blogger.