Trending News>>

JIFUNZE KWA KUSOMA SIMULIZI MBALIMBALI

SIMULIZI: DOKTA SIUMWI HUKO
SEHEMU:  YA TATU 
MTUNZI: MR ManyamaJr
MAWASILIANO: 0767464766




ILIPOISHIA:
"Kwani mmehangaika kwa muda mrefu sana anti?"
"Yaani wee acha tu dokta, ikishindikana na hapa itabidi niridhike tu kuwa sikupangiwa kuzaa kabisa"

"Ndoa yenu ina muda gani sasa?," Dokta Kisarawe alizidi kumdadisi Sulee huku muda nao ukizidi kuyoyoma na tayari saa iliyokuwa ukutani ilisomeka saa mbili na dakika nne.
"Miaka mitatu sasa dokta"

"Mm..!"

"Mbona unaguna dokta jamani, au huamini?"


TIRIRIKA NAYOO...
"Hapana anti, naguna kwa kushangaa mwanamke mzuri kama wewe hujapata mtoto!," alijibu Dokta Kisarawe huku akimkazia macho Sulee hasa maeneo ya kifuani na mapajani kutokana na sketi aliyokuwa amevaa kupanda hadi kuvuka juu ya magoti.

"Kwani mimi mzuri ja..ma..ni;?," aliuliza Sulee lakini safari hii kwa sauti iliyokatakata.

"Dah! Wewe ni mzuri sana anti, nashangaa hadi sasa hujapata mwanaume wa kukupa mimba;!"

Hapo Sulee hakusema neno zaidi ya kuendelea kumtumbulia macho Dokta Kisarawe aliyekuwa bize na kumungalia.

Alipoona Sulee yuko kimya, Dokta Kisarawe akazidi kumsifia huku akimhakikishia ni lazima atapata mimba.

"Yaani mwanamke umeumbika haswa, ona maeneo kama haya ya kifuani jamani," Dokta Kisarawe aliendelea kumchombeza Sulee huku sasa akionesha kwa vitendo na kuyagusa maeneo ya kifuani ya mwanamke huyo mrembo wa sura na umbo achilia mbali rangi yake ya chokoleti.

"Kweli; kwelii dokta jamani?," Sulee aliuliza kama kweli anaweza kuzaa lakini kwa sauti ya mkwamo kutokana na mkono wa dokta kugusa maeneo nyeti ya kifuani.

"Duh! yaani anti na nido nzuri kama hizi halafu huzai!"

"Mm!," Sulee aliishia kuguna huku akijikunja kiaina kwani safari hii vidole vya dokta viligusa kisawasawa nido zake kutokana na blauzi nyepesi aliyoivaa mwanamke huyo.

"Hujapata tu mwanaume rijali;"

"Kwa nini unasema hivyo dokta jamani;," Sulee aliuliza katika hali ya kutojiweza, huku macho yake yakianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kiasi.

"Mimi ni daktari si kwa matokeo ya mtihani bali kwa kukidhi vigezo, ina maana nina uwezo wa kujua tatizo la mgonjwa hata kwa saikolojia tu, yaani wewe unahitaji mwanaume rijali tu, kweli tena nakuambia," Dokta Kisarawe alizidi kutoa maelekezo kwa vitendo zaidi na safari hii mikono yake ikiparaza juu ya mapaja ya Sulee.

"Aah! Sasa huyo mwanaume rijali nitampata wapi jamani mbona haya ni majaribu sana dokta?"

"Kha! Mbona wapo wengi sana, huko mitaani au hata mimi;"

"Mimi wa mitaani naogopa, mume wangu ni mkorofi sana

"Basi mimi" Dokta Kisarawe alipasua ukweli wake huku mikono yake ikiwa na kazi ya kumpapasa na kumbinya kimtindo Sulee, kuanzia maeneo ya kifuani, mapajani hadi mgongoni na kumalizia kwenye kiuno kipana na cha mviringo cha mwanamke huyo.

Kutokana na joto la mikono ya dokta, Sulee alikuwa akipeleka upinzani hafifu na kuruhusu mikono hiyo izidi kutalii kadri iwezavyo na kumuacha akilalamika kimahaba huku akitamka maneno ya kukolea penzi.

"Aaah, jamani dokta lakini mimi siumwi huukooo" Sulee alilalama huku akitoa ushirikiano kwa dokta.

Baada ya kuona amekolea, Dokta Kisarawe hakuwa na ajizi zaidi ya kumuandaa na kumsogeza hadi kwenye kitanda kilichotumika kwa wagonjwa kulazwa wakiwemo wale wa kujifungua.

Dakika chache kila mtu akawa ameiva na kuhitaji kukabiliwa na mwenzake, vilio na miguno ya kimahaba vikatawala ndani ya chumba hicho cha Dokta Kisarawe.

Haikuchukua muda mrefu, Sulee akatangaza kufika mwisho wa safari na dokta akimkaribisha kwa bashasha zote.

Baada ya shughuli pevu, dokta alimtaka Sulee arudi siku ya kesho kwa ajili ya vipimo zaidi kwa wakati huo, muda ulikuwa umekwenda.

"Ahsante sana dokta jamani, wewe ni tofauti sana," alisema Sulee baada ya kuagana na dokta na kisha kuondoka huku akiangalia nyuma.


***********
Masofa ambaye ni mume wa Sulee alikuwa sebuleni akimsubiri mkewe ambaye alichelewa sana kurudi kutoka kwa dokta.

"Ina maana huyu hadi sasa ni tiba gani hiyo;," alijiuliza Masofa akiwa na hasira.

Wakati akiwaza hayo, alisikia hodi na kwenda kufungua akakuta ni mkewe.

"Jamani mke wangu Sulee, hadi saa hizi ulikuwa kwa dokta tu?"

"Sasa kumbe nilikuwa wapi tena jamani mume wangu;?," alijibu Sulee huku akitupia mkoba wake kwenye kochi.

"Dokta alikuwa na watu wengi, ndiyo maana nimechelewa kwani sasa hivi saa ngapi?"

"Angalia saa mwenyewe;"
"Mm! yaani saa tano kasoro mara hii;!"
"Haya, niambie huyo dokta amesema nini?"
"Kwa leo amenipa ushauri tu wa kisaikolojia, amesema nirudi tena kesho muda kama wa leo;," alijibu Sulee.
"Mm!, ina maana leo amekupa ushauri tu?"
"Ee mume wangu;"

"Inabidi kesho twende wote," alisema Masofa na kumuacha Sulee ametumbua macho.

ITAENDELEA.....!! JE MASOFA AMESHTUKIA MCHEZO? VIPI MKEWE ATAKUBALI KWENDA NAE? USIKOSE SEHEMU YA NNE.

No comments:

Powered by Blogger.