Trending News>>

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 91 & 92(Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA 

ILIPOISHIA
Madam Mery akanitazama kwa muda, huku akikoaa cha kuzungumza, taratibu nikaanza kukichomoa kisu changu kilichopo kwenye soksi ya mguu wa kushoto, kwa ajili ya kuikata shingo ya madam Mery aliye, nifanyia ukatili mkubwa, akishirikiana na washenzi wezake John na Victoria.
ENDELEA
   Shamsa akanishika mkono, ulio kua ukichomoa kisu kutoka katika soksi. Akanikonyeza huku akinionyesha camera ya ulinzi, iliyopo kwenye moja ya kona ya ukuta wa ofisi hii. Nikakirudisha kisu nilipo kitoa. Nikabaki nikimtazama madam Mery kwa macho makali, yaliyo jaa hasira. 
"Eddy ninatambua kwamba una hasira na mimi"
Madam Mery alizumgumza na kukaa kimya huku, akiyakwepesha macho yake kutazamana na macho yangu.
"Sikupenda kufanya kile walicho kufanyia John na nwenzake. Roho yangu iliniuma sana pale nilipo sikia kwamba umekufa."
Madam Mery alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Shamsa akasimama na kupiga hatau hadi mlangoni.
"Eddy nipo nje ninakusubiri"
Nikamuitikia Shamsa kwa kutingisha kichwa kumuashiria kwamba nimekubali yeye kutoka nje ya ofisi. Madam Mery akatoa kitamba kwenye pochi yake na kujifuta machozi yaliyo tapakaa usoni mwake.
'Huyu mnafki kweli"
Nilijiseme kimoyo moyo huku nikimtazama madam Mery usoni mwake.
"Eddy moyo wangu ulikosa amani, nilijaribu kutafuta japo kaburi lako, nije nipige magoti nikuombe msamaha"
"Ila sikuweza kufanikiwa katika hilo, ila nilikuka kupta amani pale nilipo kuon kwenye tangazo la magari, ndipo nilipo tambua kwamba upo hai"
Madam Mery alizumgumza huku alinyanyuka kwenye kiti chake na kuja nilipo. Akapiga magoti chini, na kuushikilia mguu wangu wa kulia, huku aliendelea kulia kwa uchungu.
"Eddy ninakupenda sana, ndio maana nilikupa nafasi ya kuishi tena duniani"
"Nakuomba unisamehe, ninakuomba unipe nafasi ya msamaha wako, ili niweze kuishi kwa amaani"
Suti ya uchungu, na yamajozi ya Madam Mery ikaanza kuilainisha hasira yangu, iliyo ganda kama barafu. Nikamnyanyua na tukasimama, akanikumbatia kwa nguvu huku akiendelea kutoa kilio cha kujutia makosa aliyo yafanya. Japo hasira bado inanisukuma niweze kumfanyia madam Mery jambo la ukatili, ila nikazidi kujitahidi kuweza kuepukana na kufanya tukio lolote baya.
"Eddy nisamehee'
Madam Mery aliendelea kuzungumza huku akilia kwa uchungu. 
"Ni...mekusamehe"
Nilijitahidi kukifungua kinywa changu, kujibu nilicho mjibu Madam Mery, japo muda sote kinatetemeka kwa hasira kali. Taratibu Madam Mery akaniachia, na kunitazama machoni mwangu. Tukabaki tukiwa tumetazamana kama dakika tatu, hisia kali ya mapenzi iliyo pelekea kuyakumbuka matukio kadhaa ya nyumà dhidi ya penzi letu, na madam Mery. Zikanifanya mwili mzima kusisimka, taratibu ñikaupelekà mdomo wangu, ulipo mdomo wa Madam Mery ila akaukwepesha usikutane na mdomo wangu.
"Eddy sio sasa"
Madam Mery akanichia na kurudi, kilipo kiti chake, nikabaki nikiwa nimemtazama kwa mAcho yaliyo jaa matamanio mengi.
"Umetuletea pesa nini?"
"Eheee!"
Nilibaki nikiwa nimemshangaa Madam Mery, huku hisia za mapezi, zikiupelekea mwili wangu kuishiwa kabisa na nguvu. Taratibu nikakaa kwenye kiti changu.
"Eddy sio kwa sasa, hiyo kamera hapo juu ukutani inarekodi kila kitu kinacho endelea humu ndani."b
Madam Mery alizungumza huku, akinionyeshea kamera iliyopo ukutani.
"Ni pesa ulizo beba?"
"Eheeee"
"Una akaunti ya benki hii?"
"Ndio"
"Hembu nitajie"
Nikamtaji madam Mery namba ya akaunti yangu, akaiingiza kwenye computer iliyopo hàpa mezani mwake. Baada ya muda akanigeuzia kioo cha çumputer hii, aina ya 'DELL'. Nikaona taarifa za benki yangu, ikiwemo picha na jina langu kamili.
"Ila inaonyesha kwa Tawi la Tanzania umefungiwa, kwa nini?"
"Ahaaa ni mama, ndio alinifungia"
"Sawa, ngoja nimpigie simu muasibu"
Akampigia simu muasibu wake kwa kupitia simu ya mezani. Tukiwa tunamsubiri muàsibu madam Mery akanipatia kokadi chenye namba ya simu yake.
"Mimi nitakwenda kwenye kikao, kama utaondoka pasipo kuonana na mimi basi utanipigia kuniambia ni wapi ulipo"
"Sawa"
Akaingia jamaa mrefu, mweusi kiasi aliye valia suti, nikatoka naye ofisini na kwenda kwenye chumba chenye mashine za kuhifadhia pesa. 
Zoezi la kuzihesabu pesa likaanza, halikuchukua muda sana tukawa tumepata kiwango cha pesa ambacho ni dola za kimarekani milioni saba. Sawa na bilioni kadhaa kwa pesa ya tanzani. Nikatoa dola laki moja na nyingine zilio salia zikaingizwa kwenye akaunti yangu.
"Eddy hatuwezi kwenda kwenye kambi ya wakimbizi muda umesha pita"
Shamsa alizungumza huku tukitoka kwenye mlango wa benki.
"Kwani ni saa ngapi sasa hivi?"
"Saa tisa mchana na muda wa kuingia pale, ni kuanzia saa nne asubuhi hadi saa nanechana"
"Sasa itakuaje?"
"Ni hadi kesho"
"Nasi tutafute sehemu ya kulala"
"Sawa, ila kama ukihitaji iwe rahisi sisi kuingia ndani mwa kambi tunaweza kununua vitu kama mifuko ya mchele, sabuni, mafuta ya kupikia. Tukifika pale tunawaambia sisi tunatoa msaada"
"Wee dogo una akili sana"
Kila wazo alilo litoa Shamsa, sikulipinga. Tukaanza kazi ya kutafuta alivyo sema. Ikatulazimu kununua na nguo ambazo zitatufanya tuonekane kweli ni watoaji msaada. Ikatulazimu pia kununua gari, jengine aina ya pickup lililo tuwezesha kubeba mizigo hiyo. Tukakodi vyumba viwili kwenye hoteli moja kubwa yakitalii, iliyopo katikati ya mji wa Mogadishu, ambapo usalama wake kidogo ni wauhakika
   Mida ya saa mbili, usiku nikampigia simu madam Mery simu, nikamuelekeza sehemu nilipo. Akaniambia nimpe dakila kadhaa atafika sehemu tulipo. 
"Una uhakika utalala naye?"
Shamsa aliniuliza swali mara baada ya kuksta simu.
"Kwa niki umeuliza hivyo?"
"Kwa maana yule mama nina mjua vizuri sana"
"Ana nini?"
"Ni mke wa waziri wa fedha hapa nçhini. Na mumewe ni mmoja wa watu hatari hapa Somalia"
"Nisinge penda kukuona unajiingiza kwenye matàtizi ambayo hayakuhusu. Wewe kwa sasa jaribu kuiangalia familia yako"
Shamsa alizungumza maneno, yaliyo nifanya nibaki kimya nisijue nini cha kujibu.
"Usiku mwema nakwenda kulala, ila nilicho kueleza kiweke akilini. Tutaonana asubuhi"
Shamsa akanyanyuka, kitandani mwangu, akapiga hatua hadi mlangoni akafungua na kutoka. Nikabaki nikiwa nà msongo wa mawazo, nikiiwazia familia yangu. Kijiusingizi kikaanza kunipitia taratibu, kila nilipo jaribu kuitazama saa ya ukutani, masaa yalizidi kuyoyoma pasipo Madàm Mery kutokea.Mida ya saa sifa usiku, nikasikia mlango ukigongwa taratibu. Nikanyanyuka, nikiwa nimeishika bastola yangu, iliyopo chini ya mto. Nikasimama pembeni ya mlango.
"Nani?"
Niliuliza kwa sauti ya chini, ambayo mtu aliyopo nje ya chumba ataisikia vizuri.
"Mery"
Ilikua nisauti ya Madam Mery nikashika funguo, iliyopo kwenye kitasa nikaizungusha tatatibu, huku nikiwa makini kwa lolote litakalo jitokeza. Nikaufungua mlango, nikakuta Madam Mery akiwa amevalia baibui jeusi, bila ya salamu kaingia ndani. Nikachungulia nje kwenye kordo, hapakuwa na mtu. Nikafunga mlango.
   Madam Mery akanikumbatia kwa furaha, huku akihema mihemo yenye pumzi moto, iliyo katiza mara kadhaa kwenye shingo yangu. 
"Mbona umeche......."
Madam Mery akaniwahi kuninyonya mdomo sangu, na kuikatisha sentensi yangu. Fukuto zito la mzhaba likatukamata miiili yetu. Nikalivua baibui la Madam Mery na kulitupa kando. Tukaendelea kunyonyàña midomo yetu, nikamnyanyua na kumuweka kitandani, tukasndelea kupeana burudani za mwili.
Saa kumi alfajiri Madam Mery akastuka, kutoka usingizini, baada ya kupitiwa na uchovu wa penzi zito tulilo peana usiku mzima.
"Unakwenda wapi?"
"Nyumbani"
"Usiku wote huu?"
"Kuna kazi nakwenda kuifanya"
Madam Mery alizungumza kwa wasiwasi, huku akiingia bafuni, akaoga na kurudi chumbani, Akavaa haraka sana, akanifwata kitandani, akanipiga busu mdomoni.
"Kesho Eddy"
Madam Mery akatoka haraka, hadi nikabaki nikishangaa.Saa kumi na mbili Sahamsa akaingia chumbani.
"Eddy za kazi"
"Kazi?"
"Ndio kazi uliyo ifanya jana usiku na mtu wako?"
Nikastuka, Shamsa akatoa simu, niliyo mnunulia jana, akanirushia kitandani. Nikaona video ya jinsi madam Mery alivyo kuja, chumbani kwangu Nikichungulia na kuufunga mlango.
"Huyo ni mimi niliye rekodi hiyo video, pasipo nyinyi kujijua. Piga picha siku wakiwa ni watu wa huyo waziri, itakuaje?"
"Jibu unalo, siñà haja ya kukusimulia kitakacho tokea. Amka twende tulipo panga"
Nikajikuta nikianza kumuogopa Shamsa, sikukua kama atanifwatilia kwa ukaribu kiasi hichi. Nikajiandaa, tukalata kifungua kinywa na kuelekea ilipo kambi ya wakimbizi, huku Shamsa akiwa ndio dereva.
Gafla Shamsa akafunga breki kali, huku akijitahidi kumkwepa mtu aliye lazwa barabarani akionekana hajitabui. Gari, likafanikiwa kusimama. 
"Eddy usishuke, hili eneo sio salama"
"Ngoka kwanza"
Nikavua koti langu la suti, pamoja na tai. Nikaichomoa bastola yangu na kuanza kutembea kwa tahadhari, kwenda alipo lala mtu huyo, huku macho yangu yakiwa makini kila sehemu. Nikafika sehemu alipo mtu huyo. Kwakutumia mguu nikamgeuza. ili niione sura yake, kutokana amelala kifudi fudi. Moyo ukanipasuka baada ya kukuta ni Amina rafiki wa Mnka, akiwa ameuawa kikatili, huku macho yake mawili yakiwa yameng'ofolewa
 ****SORRY MADAM***(92)

  Huku yakitoka funza wadogo wadogo, harufu kali ya mwili wa Amina, haikunizuia kuchuchumaa kumtazama vizuri. Mwili wake tayari umeanza kuharibika kutokana na kujeruhiwa vibaya kwa mapanga, sikuweza kuusogeza pembeni ya barabara, kutokana na baadhi ya nyama za mwili wake, kushikamana na barabara hii ya lami. Nikajikuta machozi yakianza kunilenga lenga, nikatazama pande zote ya eneo tulilopo hapakuwa na dalili yoyote ya mtu kutokea zaidi ya Shamsa aliye simama, nje ya gari letu akinitazama kwa kitu ninacho kifanya.
   Nikazidi kujihisi uchungu baada ya kukisogeza kichwa cha Amina kwa kutumia bastola yangu, na kukuta ubongo wote ukiwa nje. Huku sehemu ya pembeni, upande wa kushoto ikiwa imepasuliwa vibaya mno.
"Ahaaa"
Nikajikuta nikitoa sauti ya uchungu, huku nikisimama. Wasiwasi ukaanza kunijaa moyoni mwangu, wa kwanza kumfikiria ni mke wangu Phidaya, ambaye kwa mara ya mwisho alikua na Amina, ambaye ni huyu amelala hapa barabarani, akiwa tayari ni mfu. Nikaanza kupiga hatua za taratibu kurudi kwenye gari. Nikafungua mlango wa gari pasipo kumsemesha chochote Shamsa, ambaye naye aliingia ndani ya gari na kuliwasha. Akanitazama kwa muda jinsi machozi hanavyo nitiririka kwenye mashavu yangu pasipo kutoa mlio wowote wakulia. Akawasha gari na kuondoka eneo hili taratibu.

  Mwendo wa takribani lisaa lizima, sikufungua kinywa changu kuzungumza na Shamsa, ambaye mara kwa mara aliniita pasipo kumjibu chochote. Akasimamisha gari kwenye moja ya sheli ya mafuta. Akashuka na kuzungumza na muuzaji wa mafuta kisha yeye akaingia kwenye duka lililopo hapa kwenye sheli. Picha kadhaaa, za Amina alivyo nisaidia kwenye tukio la kuiokoa familia yangu, zikaanza kunijia kichwani. Hadi picha ya mwisho ya mwili wake, ulio haribika ndio ikagota kwenye ubongo wangu, unao shuhulka na kumbukumbu. Nikaichomoa bastola yangu haraka na kuinyoshea kwa mtu aliye chungulia kwenye kioo cha upande wa Shamsa.
"Ohhhhhhhh"
Sauti ya dada, muhudumu wa sheli hii, niliisikia. Macho yake akawa meyatoa kwenye bastola niliyo mnyooshea. Nikamuona jinsi anavyo tetemeka kwa woga. Jasho jingi likaanza kunimwagika. Huku nikiyang'ata meno yangu kwa hasira kali, iliyo changanyika na uchungu wa kutamani kulipiza kisasi kwa yeye aliye muua Amina.
"Eddy unafanya nini?"
Shamsa alizungumza huku akiufungua mlango wa gari, akausogeza mkono wangu pembeni ulio shika bastola. Akaweka bidhaa alizo zinunua siti ya nyuma.
"Samahani dada, pesa yako hii hapa."
Shamsa alizungumza huku akimpa dada huyo, pesa anayo dai kwa mafuta aliyo tuwekea kwenye gari. Shamsa akafunga kioo, akawasha gari na tukaondoka.
"Eddy unatatizo gani, nji nzima unakazi ya kumwagikwa na machozi, nakuuliza hutaki kunijibu?"
Shamsa liniuliza kwa sauti ya ukali, huku akinikodolea macho. Nikairudisha bastola yangu nilipo ichomoa kwenye kiuno, ilipo kua imebanwa vizuri kwa mkanda wangu wa suruali.
"Geuza gari turudi, kwenye ule mwili"
"Nini, hivi Eddy umechanganyikiwa?"
Shamsa alizungumza huku, akifunga breki za gari na kulisimamisha kando ya barabara.
"Nimekuambia geuza gari turudi, kwenye ile maiti."
"Eddy tumia akili, mtu humjui, ya nini kujifanya msamaria mwema, kwa matatizo yasiyo yako. Tumebakisha kilomita moja tufike, wewe unataka turudi tena kilomita ishirini nyuma? Ahaaa siwezi kufanya ujinga kama huo."
Shamsa alizumgumza kwa kujiamini sana. Nikamtazama kwa macho makali yaliyo jaa hasira na uchungu. Nahisi atambui ni nini anazungumza.
"Tunarudi au haurudi?"
Ilinibidi na mimi kuzungumza kwa sauti ya hasira, iliyo mstua Shamsa, ambaye kwa kipindi kifupi nilicho kaa naye, amenizoea sana.
"Eddy, fikiria juu ya familia yako, fikiria juu ya mwanao na mkeo. Kwa nini unataka kufanya vitu vitakavyo kuhatarisha usalama wako, na kukutenga na familia yako?"
"Fikiria hilo, hii nchi haina usalama kama umavyo fikiria wewe, jiulize yule ni kwanini amuauwa na kutupwa pale barabarani, piga picha ni mimi au wewe ndio tumetupwa pale barabarani, utajihisi vipi?"
Shamasa alizungmza kwa sauti ya upole huku machozi yakimwagika, nikabaki niliwa ninafikiria ni nini cha kufanya. Sikuwa na uwezo wa kuhairisha safari ya kwenda kwenye kambi ya wakimbizi ilipo familia yangu, na kurudi kuuchukua mwili wa Amina ambao tayari umesha haribika vibaya mno, na hata niiuchukua nisingeweza kuuzika leo, pia endapo polisi watanikamata na mwili huu, wataniweka kuzuizini hadi watakapo fanya uchunguzi ambao sijajua utachukua muda gani kukamilika.
"Eddy, natambua wewe ni mtu mwema. Ila si kwa kila kitu unatakiwa kufanya wema, mengine inapo kupasa kufanya ukatili fanya hata kama mtu unamtambua. Ila kama atakuwa adui yako wewe fanya kwani ukimuacha atakudhuru wewe"
Shamsa alizungumza maneno yaliyo nifanya nianze kukata tamaa, juu ya mwili wa Amina, uliopo barabarani.
"Washa gari tuendelee na safari"
Shamsa akafanya kama nilivyo muagiza. Safari ikaendelea.
"Kwani unamtambua marehemu?"
"Ndio"
"Eheeee ni nani yako!?"
"Anaitwa Amina, ndio aliye nisaidia katika kuiokoa familia yangu, hadi ikachukuliwa na jeahi la umoja wa mataifa. Na wakapelekwa kwenye hiyo kambi ya wakimbizi kwa usalama wao zaidi"
"Mmmm, kuna kitu kinacho endelea hapa. Kuwa makini Eddy. Yaani hii nchi anaye kuua huwezi kumdhania kabisa. Laiti ningeamua kukuua mimi si ningekuua siku tulivyo kutana. Ila uliniacha kwasababu ni mtoto."
"Ndio"
"Ndio unatakiwa kuwa makini, na hata watoto wadogo, kwani huku watoto pia wamepandikizwa roho za chuki na ugaidi"
"Ile nyumba iliyo lipuka ni ya yule dada, aliye uwawa"
"Weee, acha utani!?"
"Utani wa nini sasa?"
"Ndio ukweli huo."
"Mungu ailaze mahali pema, roho ya marehemu"
"Amin"

  Taratibu nikaanza kupata picha ya siku nilivyo rudi, nyumbani mwa Amina na kukuta mwili wa askari aliye kufa. Wasiwasi ukazidi kuongezeka baada ya kumkumbuka Manka, ambaye tulimuacha kwenye nyumba ya Amina na sikumkuta na hadi sasa hivi sifahamu ni wapi alipo.
"Ngoja niipate familia yangu kwanza"
Nilizungumza, huku Shamsa akisimamisha gari, kwenye megesho ya nje ya geti, la kuingilia katika kambi ya wakimbizi.
Tukaacha bastola zetu ndani ya gari, tukashuka na kwenda kwenye kijumba kidogo, kilicho jengwa kwa ajili ya ofisi ya wanajeshi wanao simama getini, kuangali ni nani anaye ingia na kutoka ndani ya kambi hii. Wakatukagua kabla ya kuingia kwenye ofisi hiyo. Kisha wakaturuhusu kuingia ndani ya ofisi, baada ya kuridhishwa na kutukagua kwetu.
"Mumesema nyinyi, niwatoaji misaada si ndio?"
Mwanajeshi mmoja, alituulizaa kwa lugha ya kifaransa, huku akitutizama machoni kwa umakini.
"Ndio"
Nilimjibu kwa kujiamini, huku nikizichunguza nguo alizo vaa, zikionyesha bendera ya nchi ya Ufaransa kwenye bega la mkono wake wa kushoto, huku mkono wa kulia kukiwa na kitambaa cheupe, kilicho andikwa kwa maandishi makubwa yenye rangi nyekundu 'MP'.
"Mumetokea wapi?"
"Ohhh Eddy karibu"
Kabla sijamjibu, aliingia mwanajeshi, mwenye nyota tatu begani, wanajeshi walio kuwemo ndani ya hii ofisi wakampigia saluti. Ikanibidi kuipokea salamu yake kwa tabasamu huku nikimpa mkono. Japo sifahamiani naye, na wala sina kumbukumbu ni wapi nilionana naye.
"Jamani huyu ndio yule jamaa aliye okoa familia ya balozi wa Marekani nchini Afrika kusini."
Wanajeshi wengine wakaanza kutabasamu na kunipa mikono ya pongezi hata wale walio nisemesha kwa kifaransa, wakazungumza kingereza japo, kifaransa ninakijua kidogo. Nikatoka na mkubwa wao aliye jitambulishwa kwa jina la Jonson, tukafika lilipo gari letu. Tukapanda wote watatu. Tukaingia getini, bila ya kukaguliwa kutokana tupo na mkubwa wao huyo mwenye nyota tatu begani mwake.
Tukafika sehemu ya kitengo cha wanao pokea misaada, inayo letwa ndani ya kambi hiyo. Tukatambulishwa, na kuwakabidhi misaada yetu. Nikawaomba waniangalizia jina la Junio na Phidaya, katika orodha ya wakimbizi walio pokelewa kipindi cha hivi karibuni. Mama anaye husika na kutunza kumbukumbu za majina ya wakimbizi, akawasha computer iliyopo ndani ya ofisi hii. Akaandika jina la Junio
"Junio nani?"
"Junio Eddy"
"Yeah wametokea saba hapa"
Aliniita na kunionyesha majina hayo ya kina Junio Eddy yakiwa saba yamejipanga vizuri.
"Hembu andika jina la Phidaya"
Akaandika haraka, ila computer, ikaonyesha hakuna jina kama hilo. Nikajaribu kuandika mwenyewe ila pia jibu likawa ni moja, kwamba Phidaya hayupo, kwenye orodha hiyo.

   Tukaondoka kuelekea kwenye mahema ambayo, wanaishi wakimbizj na pis tunaweza kuwapata Junio, hema la kwanza, tukakuta Junio huyo ni mtu mzima, mwenye umri zaidi yangu. Kila Junio tunaye onyeshwa si mwanangu, kwani wote wamezidi umri wa Junio wangu. Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio, baada ya Junio sita nilio onyeshwa na sio mwanangu. Tukafika kwenye hema ambalo walidai tutampata Junio huyo mwengine waliye nieleza ni mtoto mdogo.
Tukakuta watu wengi kiasi wakiwa wamekusanyika nje ya hema hilo, huku wakiwa na huzuni machoni mwao. Muhudumu mmoja kati ya wanne tulio ongozana nao, akamfwata muhudumu, anaye onekana ni daktari aliye kuwepo nje ya hema hilo akizungumza na watu. Waka non'gonezana, na daktari huyo akatutizama, kisha akawaomba watu wanao msikiliza, wamsubiri kidogo azungumze nasi.
"Huyu ni dokta Martin, ndio mganga mkuu wa hii kambi"
Jamaa, alitutambulisha kwa dokta huyo, mwenye asili ya Uingereza na anaumri mkubwa kiasi.
"Walikua wakimuulizia Junio Eddy"
Dokta akakaa kimya kidogo, huku akinitazama machoni, Shamsa akanishika mkono wa kulia vizuri, kutonana na yeye kuchoka kwa kuzunguka kwenye kambii hii kubwa, huku jua kali likituchoma, ipasavyo.
"Ohhh Junio Eddy, tunetoka kumzika masaa mawili ya nyuma"
"Nini doktar?"
Mstuko wangu, uliwafanya hata watu walio kua wakimsikiliza doktar huyo kunigeukia mimi.
"Ndio, tulimkuta na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola, na yeye ndio mtu wa kwanza kuugua ugonjwa huo ndani ya kambi hii. Na hapo nilikua nikitoa mafunzo kwa watu wengine endapo wataona mtu mwenye dalili hizo watufahamishe haraka iwezekanavyo."
  Sikuweza kuyazuia machozi yangu kunimwagika, Shamsa akawa wa kwanza kunikumbatia kwa nguvu huku akinibembeleza.
"Mwanangu amekufa kabla sijamuona"
"Hapana Eddy ni kazi ya Mungu, jikaze usilie mbele za watu"
Shamsa alizungumza huku, akinibembeza, Shamsa akanishika mkono, tukaondoka huku nikimuacha Jonson akizungumza na daktari huyo pamoja na wahudumu, tulio kuja nao, wakionekana kustushwa na ugonjwa huo ambao ni hatari sana duniani.
"Eddy jikaze, wewe ni mwanaume. Usilie kila mmoja akajua unamatatizo"
Shamsa aliendelea kunifariji, huku tukizidi kutembea kurudi getini. Kundi kubwa la watoto, wenye umri kama miaka kumi hivi, tukalikuta limekusanyika kwenye moja ya mti, huki wakishangili watoto wawili wanao rushiana makonde. Nikajifuta machozi na kwenda walipo watoto hao, nikapita katikati yao, na kumkuta mtoto mmoja akiwa amelazwa chini, na mwenzake amwe nguvu kumpita yeye.
Nikawatennganisha, nikamnyanyua mtoto aliye chini, ambaye sura yake kidogo imevimba, kutokana na kichapo hicho.
"Musipigane sawa, watoto wazuri"
Nilijikaza tu, kuzungumza hivyo. Sikutaka kuwataza machoni watoto hawa, ili wasigundue kwamba ninalia. Nikapita kati kati yao, nikabaki nikimshangaa Shamsa, akiwa ameduwaa, akiwatazama watoto hao.
"Shamsa twende"
"Eddy ngoja"
Shamsa alizungumza, huku akipiga hatua akipita katikati ya watoto hao. Akamfikia yule aliye pigwa, anaye onekana kuvimba sura yake. Akamtazama vizuri, kisha akanitazama na mimi.
"Eddy"
"Mmmm"
"Huyu ni mwanao"
Shamsa alizungumza, huku akimtazama mtoto huyo, niliye anza kumtazama kwa umakini.
"Mtoto unaitwa nani?"
Shamsa alimuuliza mtoto huyo, ambaye na mimi nikaanza kupata mashaka naye, japo sura yake imevimbishwa kwa ngumi za mwenzake na kuifanya iumuke kiasi, ila anafanana kidogo na mimi.
"Jack"
Kulitaja jina la Jack, maumivu ya kufiwa na Junio wangu yakarudi upya, kwani hakuwa Junio wangu.
"Jack nani?"
"Mama hajaniambia baba yangu anaitwa nani"
"Mama yako, yupo wapi?"
"Yupo kule, ninapo kaa"
"Twende ukatuonyeshe"
Shamsa akamshika Jack mkono na kuongozana naye.
"Eddy twende, umashangaa nini?"
Shamsa aliniambia kwa sauti ya chini, nikawafwata kwa nyuma, huku nikimchunguza vizuri mtoto huyu kwa nyuma. Sikutaka kuwema asilimia mia kwamba ni mwanangu, kwani tayari amesha nichanganya, kwa jina lake la Jack. Tukaona moshi mwingi, ukienda juu. 

Ukitokea kwenye mahema ya mbele yetu, Jack akajichomoa mikononi mwa Shamsa na kuanza kukimbia kuelekea moto ule unapo tokea. Ikamlazimu, Shamsa naye kumkimbiza kwa nyuma, mimi sikuwa na hata nguvu za kukimbizana nao, zaidi yakuwafwata kwa nyuma. Wakawahi kufika kwenye mahema yanayo ungua kwa moto. Nikafika na kumkuta Jack akilia huku akimuita mama yake, ambaye anahisi yupo ndani ya hema hilo. Huku watu wengine wakiendelea kuzima moto kwa kutumia mchanga, kwani hapakuwa na moto wa kufanyia hivyo.
"Jack, Jack"
Sauti ya msichana, ilisikika nyuma yangu, kabla sijageuka, kumtazama dada huyo nikajikuta nikipigwa kikumbo kwa nyuma, dada huyo akanipita na kukumbatia na Jack, huku dada huyo akinipa mgongo, na sikuiona sura yake. Tukabaki tukitazamana na Shamsa, huku mimi nikiwa sina la kuzungumza.
"Ulikuwa wapi mwanangu"
Sauti ya dada huyu, ikazidi kunipa ushawishi wa kutaka kumgeuza, ili kuiona sutmra yake kwani inaendana na sauti ya Phidaya, japo imejaa mikwaruzo mingi, kama mtu ansye ugua kifua kikali.
"Nilikua na hao hapo.'
Jack akanyoosha kidole kwangu, na kumfanya mama yake anigeukie. Phidaya, akanitazama kwa mshangao mkubwa, huku machozi yakianza kumlenga lenga. Kukondeana kwa Phidaya, kumembadili sana, muonekano wake. Mashavu yake yameingia ndani, akionekana kukosa lishe bora kwa muda mrefu. Mavazi aliyo yavaa, yanechakaa, sana na  yanazidi kumuonyesha anamatatizo mengi, nywele zake za ndefu, zimejaa masponji mengi, ya godoro alilo lalia. Kiufupi Phidaya amechakaa sana kwa shida alizo pitia.
Taratibu Phidaya akasimama, akanisogelea huku machozi yakimwagika. Nikataka kumkumbatia, ila akanizuia, nisifanye hivyo. 
"Phida.."
Kofi zito kutoka kwa Phidaya likatua shavuni mwangu, lililo mfanya Shamsa kustuka. Phidaya akaachia msunyo mkali na kumshika mkono Jack.
"Junio tuondoke"
Phidaya alizumgumza kwa hasira, na kuanza kuondoka na mwanaye, wakijichanganya katikati ya watu walio kusanyika hapa.

==> ITAENDELEA

No comments:

Powered by Blogger.