Trending News>>

Model Calisah Afunguka Baada ya Kusambaa Kwa Video yake Akimla ‘Denda’ Wema Sepetu

Weekend hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa video inayomuonyesha malkia wa filamu nchini Wema Sepetu akiliwa denda na model Calisah.

Wawili hao ambao walitumia nguvu nyingi kufanya siri mahusiano yao, wameumbuka kupitia video hiyo iliyosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Calisah amesema hajui ni nani ambaye amesambaza video hiyo mtandaoni kwani walikuwa nayo yeye pamoja na Wema.

“Nilikuwa nachati na Wema kawaida ghafla nikaona notification, kufungua ndio nikakuta hiyo video na mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kumuuliza Wema kwa sababu video nilikuwa nayo mimi na Wema,” alisema Calisah.

Pia model huyo amedai video hiyo imemsababishia matatizo katika familia yake pamoja na kumpoteza bibi yake kwa presha

No comments:

Powered by Blogger.